Lissu ashinda uenyekiti Chadema – Mbowe

January 22, 2025 9:00 am · Nuzulack Dausen
Share
Tweet
Copy Link
  • Hadi sasa matokeo rasmi ya uchaguzi huo hayajatangazwa ila Mbowe ameshakubali kushindwa.

Dar es Salaam. Mwanasiasa machachari wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Tundu Lissu amechaguliwa na wajumbe wa mkutano mkuu wa chama hicho kuwa mwenyekiti akimbwaga kiongozi wa muda mrefu, Freeman Mbowe. 

Lissu, aliyekuwa makamu mwenyekiti wa Chadema, alikuwa akichuana vikali na Mbowe ambaye amekiongoza chama hicho kikuu cha upinzani nchini Tanzania kwa zaidi ya miaka 20. 

Mbowe ameeleza katika ukurasa wake rasmu wa mtandao wa X kuwa amepokea kwa mikono miwili maamuzi ya uchaguzi wa mkutano mkuu wa chama chao uliohitimisha leo asubuhi. 

“Nampongeza Mheshimiwa Tundu Lissu na wenzake kwa kuaminiwa kutwikwa jukumu la uongozi wa chama. Nawatakia kila la kheri katika kukipeleka mbele chama chetu,” amesema Mbowe. 

Hadi sasa bado wasimamizi wa uchaguzi huo bado hawajatoa matokeo rasmi ya uchaguzi huo licha ya wagombea kueleza matokeo ya awali. 

https://twitter.com/freemanmbowetz/status/1881934288486125740
Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

Nukta TV

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Nukta TV

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

Nukta TV