Lissu ashinda uenyekiti Chadema – Mbowe

January 22, 2025 9:00 am · Nuzulack Dausen
Share
Tweet
Copy Link
  • Hadi sasa matokeo rasmi ya uchaguzi huo hayajatangazwa ila Mbowe ameshakubali kushindwa.

Dar es Salaam. Mwanasiasa machachari wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Tundu Lissu amechaguliwa na wajumbe wa mkutano mkuu wa chama hicho kuwa mwenyekiti akimbwaga kiongozi wa muda mrefu, Freeman Mbowe. 

Lissu, aliyekuwa makamu mwenyekiti wa Chadema, alikuwa akichuana vikali na Mbowe ambaye amekiongoza chama hicho kikuu cha upinzani nchini Tanzania kwa zaidi ya miaka 20. 

Mbowe ameeleza katika ukurasa wake rasmu wa mtandao wa X kuwa amepokea kwa mikono miwili maamuzi ya uchaguzi wa mkutano mkuu wa chama chao uliohitimisha leo asubuhi. 

“Nampongeza Mheshimiwa Tundu Lissu na wenzake kwa kuaminiwa kutwikwa jukumu la uongozi wa chama. Nawatakia kila la kheri katika kukipeleka mbele chama chetu,” amesema Mbowe. 

Hadi sasa bado wasimamizi wa uchaguzi huo bado hawajatoa matokeo rasmi ya uchaguzi huo licha ya wagombea kueleza matokeo ya awali. 

https://twitter.com/freemanmbowetz/status/1881934288486125740
Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Aug, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Aug, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Aug, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Rais Samia: AFCON ni fursa, wawekezaji karibuni kuwekeza

Rais Samia: AFCON ni fursa, wawekezaji karibuni kuwekeza

Nukta TV

Utani wa Rais Samia, matokeo kati ya Simba na Yanga

Utani wa Rais Samia, matokeo kati ya Simba na Yanga

Nukta TV

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Nukta TV