Lissu ashinda uenyekiti Chadema – Mbowe

January 22, 2025 9:00 am · Nuzulack Dausen
Share
Tweet
Copy Link
  • Hadi sasa matokeo rasmi ya uchaguzi huo hayajatangazwa ila Mbowe ameshakubali kushindwa.

Dar es Salaam. Mwanasiasa machachari wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Tundu Lissu amechaguliwa na wajumbe wa mkutano mkuu wa chama hicho kuwa mwenyekiti akimbwaga kiongozi wa muda mrefu, Freeman Mbowe. 

Lissu, aliyekuwa makamu mwenyekiti wa Chadema, alikuwa akichuana vikali na Mbowe ambaye amekiongoza chama hicho kikuu cha upinzani nchini Tanzania kwa zaidi ya miaka 20. 

Mbowe ameeleza katika ukurasa wake rasmu wa mtandao wa X kuwa amepokea kwa mikono miwili maamuzi ya uchaguzi wa mkutano mkuu wa chama chao uliohitimisha leo asubuhi. 

“Nampongeza Mheshimiwa Tundu Lissu na wenzake kwa kuaminiwa kutwikwa jukumu la uongozi wa chama. Nawatakia kila la kheri katika kukipeleka mbele chama chetu,” amesema Mbowe. 

Hadi sasa bado wasimamizi wa uchaguzi huo bado hawajatoa matokeo rasmi ya uchaguzi huo licha ya wagombea kueleza matokeo ya awali. 

https://twitter.com/freemanmbowetz/status/1881934288486125740
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Wabunge waliokwenda Morocco bila kibali kikaangoni , utoro ukiibuliwa bungeni

Wabunge waliokwenda Morocco bila kibali kikaangoni , utoro ukiibuliwa bungeni

Nukta TV

Mfahamu Leonard Mususa Alama ya Ungozi iliyoacha majonzi kwa 'MACEOs' Tanzania

Mfahamu Leonard Mususa Alama ya Ungozi iliyoacha majonzi kwa 'MACEOs' Tanzania

Nukta TV

Bei za mafuta mwezi Juni hizi hapa, dizeli ikipaa kwa Sh85

Bei za mafuta mwezi Juni hizi hapa, dizeli ikipaa kwa Sh85

Nukta TV