Mwanzo, mwisho wa Malkia Elizabeth II wa Uingereza

September 9, 2022 11:33 am · admin
Share
Tweet
Copy Link
  • Ndiye mtawala wa muda mrefu zaidi katika historia.
  • Sasa Uingereza kuwa na mfalme mwanamke baada ya miaka 70 kupita.

Dar es Salaam. Hatimaye mara baada ya kuwa mtawala wa juu kabisa wa Taifa la Uingereza kwa muda wa miaka 70 na siku 274, Malkia Elizabeth wa pili amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 96.

Taarifa za kifo cha malkia kilichotokea katika jumba lake huko Uskoti  zilichapishwa katika ukurasa rasmi wa Twita  wa familia ya kifalme jana Septemba 8, 2022. 

Malkia Elizabeth wa pili alishika wadhifa huo mwaka 1952 kufuatia kifo cha baba yake Mfalme George VI na kutawazwa rasmi mwaka 1953 ambapo aliiongoza Uingereza na mataifa mengine ambapo kwa sasa yamesalia 16.

Kwa sasa viongozi mbalimbali wanaendelea kutuma salamu za rambirambi ambapo Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ameungana nao kutoa pole kwa familia ya kifalme pamoja na Uingereza kwa ujumla.

Kwa Mujibu wa taratibu za kifalme mtoto wa Kwanza wa Malkia Elizabeth II,Charles III ndiye Mfalme wa Uingereza ambapo anakuwa mfalme mwanaume baada ya miaka 70 kupita.

Follow Us on TikTok

FOLLOW NOW

Subscribe to Our YouTube Channel

SUBSCRIBE NOW