Muswada bima ya afya kwa wote wakwama tena bungeni

February 9, 2023 9:16 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Bunge lasema unahitaji kufanyiwa maboresho.
  • Utawasilishwa katika mikutano ijayo ya Bunge. 

Dar es Salaam.  Muswada wa Bima ya Afya kwa Wote ambao ulikuwa uwasilishwe bungeni leo umekwama kwa mara nyingine ili kutoa fursa ya kurekebisha baadhi ya mambo ambayo yameonekana yana upungufu.  

Spika wa Bunge Dk Tulia Ackson ameliambia Bunge leo Februari  9, 2023 jijini Dodoma kuwa muswada huo ambao ulikuwa uanze kujadiliwa bungeni leo na kesho, umerudishwa kwenye kamati ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kwa ajili ya kujadiliwa zaidi.

Dk Tulia amesema muswada wa Bima ya Afya kwa Wote umesogezwa mbele mpaka wakati mwingine ambapo kwa sasa majadiliano yanaendelea na hasa eneo la bajeti na utekelezaji wa muswada huo.

“Sasa hati hii haitawasilishwa leo mezani kwa sababu Bunge pamoja na Serikali tunaendelea na mashauriano juu ya mambo ambayo hatujaafikiana vizuri,” amesema Spika Tulia. 

Hii ni mara ya pili muswada huo kukwama tangu usomwe kwa mara ya kwanza bungeni katika mkutano wa nane wa Bunge na kupelekwa katika kamati hiyo kwa ajili ya kuchambuliwa.

Hivi karibuni Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu na watendaji wa wizara yake wamekuwa wakikutana na makundi mbalimbali ya wadau wakiwemo viongozi wa dini ili kutoa elimu na kuongeza uelewa wa bima hiyo na kupokea maoni maeneo ya kuboresha.

Huenda kukwama kwa muswada huo kutapunguza matumaini ya Watanzania kuipata bima hiyo kwa wakati ikizingatiwa kuwa watu wengi wanalalamikia gharama kubwa za matibabu wanapoenda hospitali.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA AKIHITIMISHA MAFUNZO YA UONGOZI NGAZI YA JUU, UONGOZI DARAJA LA PILI KOZI 2025/26

🔴LIVE: RAIS SAMIA AKIHITIMISHA MAFUNZO YA UONGOZI NGAZI YA JUU, UONGOZI DARAJA LA PILI KOZI 2025/26

Nukta TV

Rais Samia: Anzisheni mfuko  kuwasaidia wafungwa wenye ujuzi wanapotoka gerezani

Rais Samia: Anzisheni mfuko kuwasaidia wafungwa wenye ujuzi wanapotoka gerezani

Nukta TV

🔴LIVE: RAIS SAMIA AKIHITIMISHA MAFUNZO YA UONGOZI NGAZI YA JUU, UONGOZI DARAJA LA PILI KOZI 2025/26

🔴LIVE: RAIS SAMIA AKIHITIMISHA MAFUNZO YA UONGOZI NGAZI YA JUU, UONGOZI DARAJA LA PILI KOZI 2025/26

Nukta TV