Kiswahili kuanza kufundishwa vyuo vya Ethiopia

January 25, 2021 12:25 pm · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni baada ya Mazungumzo kati ya Rais wa Tanzania na Rais wa Ethiopia.
  • Kitaanza kufundishwa katika Chuo Kikuu Cha Addis Ababa nchini humo.
  • Walimu wa Kiswahili kuneemeka na fursa hiyo.  

Dar es Salaam. Huenda itakua ni kicheko kwa wabobezi wa lugha ya Kiswahili nchini Tanzania, baada ya Serikali kuingia makubaliano na Ethiopia ya kuanza kufundishwa kwa lugha hiyo katika Chuo Kikuu Cha Addis Ababa nchini humo.

Makubaliano hayo yamefikiwa leo Januari 25,2020 kati ya Rais John Magufuli na Rais wa Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Shirikisho la Watu wa Ethiopia, Sahle – Work Zewde aliyekuwepo nchini kwa ziara ya kikazi ya siku wilayani Chato Mkoani Geita.

“Leo tumezungumza naye amesema hili swala wala halina tatizo atapenda kupata walimu watakaoshiriki kufundisha Kiswahili katika Chuo Kikuu Cha Addis Ababa na mimi nimemshukuru sana Mheshimiwa Rais,” amesema Rais Magufuli, baada ya kumaliza mazungumzo na mgeni wake.

Kiswahili ni lugha ya Taifa ya Tanzania na baadhi ya nchi za Afrika Mashariki, ambapo kimekuwa kiungo muhimu cha shughuli mbalimbali ikiwemo biashara na utamaduni duniani.  


Soma zaidi:


Rais Zewde amesema juhudi hizo ni muendelezo wa juhudi zilizokuwepo za kuifanya lugha ya Kiswahili kama lugha ya bara la Afrika.

“Tulikuwa na mchakato wa kutaka Kiswahili kiwe lugha inayotumika Afrika. Nashukuru sana na tutakuwa tayari kuwapokea walimu kutoka Tanzania kwa ajili ya kufundisha Kiswahili Ethiopia,” ameeleza Rais wa Ethiopia.

Pamoja na fursa hiyo kwa walimu wa Kiswahili wa Tanzania, marais hao pia walipata muda wa kujadili makubaliano katika sekta za mifugo, uwekezaji, utalii na ulinzi ambayo lengo lake ni kuendelea kunufaisha nchi hizo mbili zilizo na mahusiano mazuri kwa muda mrefu.

Pia Kiswahili kinatumika kama lugha rasmi ya Jumuiya ya Maendeleo ya nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) na kinazidi kuchanja mbuga hadi jumuiya za kimataifa. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
16 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
17 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
17 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Magonjwa haya matano yanayoongoza kwa kuua watu duniani

Magonjwa haya matano yanayoongoza kwa kuua watu duniani

Nukta TV

Mambo yakuzingatia kabla ujawasha gari lako asubuhi

Mambo yakuzingatia kabla ujawasha gari lako asubuhi

Nukta TV

Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Nukta TV