Jinsi ya kuthibitisha habari za Corona unapotumia Twitter

July 25, 2020 7:46 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni kwa kutumia programu tumishi ya Twitonomy kujua tabia ya akunti ya Twitter unayotilia mashaka.
  • Itakusaidia kufahamu aina ya habari zinazochapishwa kama ni za kweli. 
  • Wakati mwingine programu hiyo inaweza isikupe matokeo unayoyahitaji. 

Dar es Salaam. Kama wewe ni mtumiaji wa Twitter na umekuwa ukikutana na akaunti ambazo una mashaka nazo kwa sababu zimekuwa zikitumika kupotosha kuhusu ugonjwa wa virusi vya Corona, basi usiwaze sana maana suluhisho lipo. 

Njia rahisi ya kufahamu akaunti feki na zinazozusha kuhusu habari za uongo zikiwemo za Corona ni kutumia programu tumishi ya Twitonomy ambayo inasaidia kufuatilia kwa ukaribu akaunti husika ili kujiweka salama dhidi ya madhara ya habari hizo. 

​Twitonomy ni zana ya kidijitali au programu ambayo hutumika kuchambua akaunti za mtandao wa kijamii wa Twitter pale unapohisi akaunti imekuwa ni chanzo cha kusambaza habari za uzushi mtandaoni.


Zinazohusiana:


Twitonomy inamuwezesha mtumiaji kujua tabia za akaunti anayoitilia mashaka ikiwemo inachapisha habari mara ngapi, nyakati gani, wafausi wake ni akina nani na inachapisha nini, ingawa matokea haya yanaweza yasiwe kwa asilimia 100.

Kitendo cha kuweza kujua tu tabia ya akunti hiyo ya Twitter itakuepusha na madhara yatokanayo na habari za uzushi. Pia ni njia rahisi ya kufahamu kama akaunti inamilikiwa na mtu au roboti. 

Kumbuka Twitonomy ni zana inayotumika unapofanya kazi za uthibitishaji habari lakini wakati mwingine inaweza isikupe matokeo unayoyahitaji kwa kiwango cha asilimia 100.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV