Jinsi kitafutio cha Google kinavyoweza kukupatia taarifa sahihi za COVID-19

February 4, 2021 8:33 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Kitafutio hicho ni bidhaa ya kampuni ya Google inayosaidia kupata vitu mbalimbali mtandaoni.
  • Kikitumika vizuri kinaweza kukupatia taarifa sahihi na kukuondolea mashaka ya uzushi wa COVID-19.

Dar es Salaam. Dunia inaenda kasi hasa katika ukuaji wa teknolojia ya upashanaji habari. Maisha yamekuwa mepesi kwa sababu taarifa zozote unazohitaji utazipata kwenye kiganja cha mikono yako.

Kwa kutumia simu janja yenye programu za vitafutio vitu mtandaoni ikiwemo “Google Search” unaweza kupata kila kitu bila kunyanyua mguu wako kutafuta taarifa kwenye ofisi za Serikali au masharika mbalimbali.

Kitafutio hicho ambacho kitakupata habari kwa namna tofauti zikiwemo picha, ramani, vitabu, nyaraka za sauti, maandishi au video, pia ni nyenzo muhimu ya kupoata taarifa sahihi kuhusu janga la Corona linaloitesa dunia kwa sasa.


Kama unataka kufahamu chochote kinachoendelea kuhusu COVID-19 unaweza kutafuta neno hilo ambalo utapata majibu ya machaguo mbalimbali na kukuwezesha kufanya maamuzi sahihi ya juu ya kujikinga na ugonjwa huo. 


Pia ipo sehemu ya picha na video ambapo utapata taarifa za picha mbalimbali kuhusu ugonjwa huo ambazo zimepigwa au kutengenezwa katika maeneo mbalimbali duniani.

Pia sehemu nyingine ambayo huwa haitumiwi na watu wengi ambayo inaweza kukupa matokeo mazuri kwenye kitafutio hicho ni sehemu ya zana (tools) ambapo zinatoa majibu mbali ya muda ambao habari imechapishwa, aina ya nyaraka unazohitaji.


Hivyo wananchi wanatakiwa kuwa makini wakati huu dunia inapambana na janga la Corona kwa kutosambaza habari zisizo sahihi na kutumia kifatutio cha Google katika kupata habari sahihi hasa wanapokutana na habari wanayoitilia mashaka.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Aug, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Aug, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Aug, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Rais Samia: AFCON ni fursa, wawekezaji karibuni kuwekeza

Rais Samia: AFCON ni fursa, wawekezaji karibuni kuwekeza

Nukta TV

Utani wa Rais Samia, matokeo kati ya Simba na Yanga

Utani wa Rais Samia, matokeo kati ya Simba na Yanga

Nukta TV

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Nukta TV