Hapana! kuoga maji ya moto siyo kinga dhidi ya Corona
- Maji ya moto hayawezi kukinga na maambukizi ya COVID-19.
- WHO imesema hata ukioga maji ya moto, joto la mwili hubaki katika hali yake ya kawaida.
Dar es Salaam. Kutokana na janga la virusi vya ugonjwa wa Corona (COVID-19) kuitesa dunia, zimeibuka dhana potofu za kutibu ugonjwa huo ikiwemo kuoga maji ya moto.
Hata hivyo, Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema siyo kweli kuoga maji ya moto kunatibu Corona kama inavyodhaniwa na baadhi ya watu.
Limesema licha ya kuoga maji ya moto, joto la mwii wako litabaki katika hali yake ya kawaida ambayo ni kuanzia sentigredi 36.5 hadi sentigredi 37.
Ikiwa utaoga maji ya moto sana, unaweza kuungua na kuishia kupata gharama za kujitibu majeraha utakayopata.
Zinazohusiana:
- Tahadhari: Epuka tovuti hizi zinazopotosha kuhusu Corona
- ‘Janga jipya la mdudu anayeua India, China’ ni uzushi
Ili kujikinga na COVID-19 unashauriwa kufuata maelekezo ya wataalam wa afya ikiwemo kukaa umbali wa walau mita moja kati yako na jirani yako, kunawa mikono kwa maji tiririka au kutumia vitakasa mikono vilivyothibitishwa.
Pia epuka kugusa pua, mdomo au macho na mikusanyiko isiyo ya lazima,
Tahadhari hizo zitakusaidia kujikinga na ugonjwa huo ambao umeenea katika nchi mbalimbali duniani.
Usiogope! Corona inazuilika na kutibika.
Latest
