Hapana: BoT haijafungua dirisha la ajira
- Benki Kuu yawataka wananchi kupuuzia taarifa hizo.
- BoT haitoi ajira zozote kwa sasa.
Dar es Salaam. Kama wewe ni mmoja wa watu waliosikia taarifa zinazosambaa mtandaoni kuwa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imefungua dirisha la maombi ya ajira, taarifa hizo si za kweli.
Taarifa hiyo inayosambaa mtandaoni kwa muundo wa picha inaonyesha muonekano wa mbele wa mfumo wa ajira wa BoT huku ikiainisha namna ya kujaza taarifa za msingi kama jina la kwanza, la pili na namba ya simu.
Mpaka sasa hakuna taarifa zozote rasmi za kuthibitisha kufunguliwa kwa dirisha hilo la ajira.
Kwa mujibu wa tovuti ya BoT hakuna ajira zozote zinazotolewa na benki hiyo kwa sasa.
“Hakuna nafasi za kazi kwa sasa. Tafadhali endelea kutembelea ukurasa huu ili kupata taarifa zaidi,” imesema taarifa kutoka kwenye tovuti hiyo.
Zinazohusiana:
Pia kupitia kupitia ukurasa wa Twitter benki hiyo wamewataka wananchi kupuuzia uzushi huo.
— Bank of Tanzania (@BankOfTanzania) December 3, 2022
Uzushi huo unasambaa kipindi hiki ambacho kuna kundi kubwa la vijana wanaotafuta ajira nchini huku taasisi mbalimbali kama Wizara ya Afya, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia zikitangaza nafasi mbalimbali za ajira.
Latest