Hapana: BoT haijafungua dirisha la ajira

December 5, 2022 1:22 pm · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Benki Kuu yawataka wananchi kupuuzia taarifa hizo.
  • BoT haitoi ajira zozote kwa sasa.

Dar es Salaam. Kama wewe ni mmoja wa watu waliosikia taarifa zinazosambaa mtandaoni kuwa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imefungua dirisha la maombi ya ajira, taarifa hizo si za kweli.

Taarifa hiyo inayosambaa mtandaoni kwa muundo wa picha inaonyesha muonekano wa mbele wa mfumo wa ajira wa BoT huku ikiainisha namna ya kujaza taarifa za msingi kama jina la kwanza, la pili na namba ya simu.

Mpaka sasa hakuna taarifa zozote rasmi za kuthibitisha kufunguliwa kwa dirisha hilo la ajira.

Kwa mujibu wa tovuti ya BoT hakuna ajira zozote zinazotolewa na benki hiyo kwa sasa.

“Hakuna nafasi za kazi kwa sasa. Tafadhali endelea kutembelea ukurasa huu ili kupata taarifa zaidi,” imesema taarifa kutoka kwenye tovuti hiyo.


Zinazohusiana:


Pia kupitia kupitia ukurasa wa Twitter  benki hiyo wamewataka wananchi kupuuzia uzushi huo.

Uzushi huo unasambaa kipindi hiki ambacho  kuna kundi kubwa la vijana wanaotafuta ajira nchini huku taasisi mbalimbali kama Wizara ya Afya, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia zikitangaza nafasi mbalimbali za ajira.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
16 Aug, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
16 Aug, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
16 Aug, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Rais Samia: AFCON ni fursa, wawekezaji karibuni kuwekeza

Rais Samia: AFCON ni fursa, wawekezaji karibuni kuwekeza

Nukta TV

Utani wa Rais Samia, matokeo kati ya Simba na Yanga

Utani wa Rais Samia, matokeo kati ya Simba na Yanga

Nukta TV

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Nukta TV