Fahamu ambayo huambiwi kuhusu chanjo ya Johnson and Johnson

July 26, 2021 3:11 pm · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Chanjo hii ni kati ya chanjo tatu zinazotolewa nchini Marekani.
  • Hadi sasa nchi zaidi ya 30 zinatumia Johnson & Johnson kama chanjo ya dharula.
  • Ni kweli awali Marekani ilisitisha chanjo hii lakini iliruhusiwa tena nchini baada ya kujiridhisha usalama wake. 

Dar es Salaam. Mengi yanazungumzwa mtandaoni kuhusu chanjo ya Johnson & Johnson ambayo ni moja ya chanjo zilizopendekezwa kutumika Tanzania.

Kwa mujibu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto chanjo hiyo ya Johnson & Johnson mashuhuri kama Janssen ni miongoni mwa aina tano ya chanjo zilizopendekezwa kutumika Tanzania ikiwa pamoja na Moderna, Pfizer, Sinopharm, na Sinovac. 

Julai 24, Tanzania ilipokea dozi ya chanjo ya Johnson & Johnson dozi zaidi ya milioni moja kutoka kwa Marekani kama msaada kupitia mpango wa chanjo kwa nchi za kipato cha chini ujulikanao kama Covax.

Serikali imesema imelenga kuchanja asilimia 60 ya watu na kwamba itakuwa ni hiari ya mtu kuchanja ama la. 

Hata hivyo, tangu chanjo hiyo iingie kuna baadhi ya watu wameachwa kwenye lindi la habari zinazopotosha kuhusu chanjo kwa ujumla ikiwemo ya Johnson & Johnson. 

Chanjo ya Johnson & Johnson inatolewa kwa zaidi ya nchi 30 duniani. Picha| Dreamstime.

Mathalani katika mitandao wa WhatsApp, baadhi wanaisema chanjo hiyo kuwa na uwezo mdogo kulinganishwa na nyingine zilizopitishwa na kuthibitishwa na Shirika la Afya Duniani (WHO), jambo ambalo si kweli. 

Wasichofahamu ni kuwa chanjo ya Johnson & Johnson ni kati ya chanjo zilizofanya vizuri zaidi katika baadhi ya nchi ikiwemo Marekani na Brazil katika kukabiliana na Uviko-19. 

Kwa Marekani ambayo inatoa chanjo aina tatu kwa raia wake, chanjo ya Johnson & Johnson imethibitishwa kufanya kazi zaidi kuliko chanjo nyingine.

Chanjo hiyo, inayotolewa kwa dozi moja kwa mpokeaji kuchomwa sindano ya kwenye misuli, imethibitishwa kufanya kazi kwa 72% nchini Marekani, 68% nchini Brazil na 64% nchini Afrika Kusini.

Baada ya kuwa na taarifa zisizo sahihi kuhusu chanjo hii, tazama video hii kufahamu vitu ambavyo wapotoshaji hawakuambii.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
20 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
21 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
21 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Prof. Mbalawa, Waziri Misri wavutana, makubaliano ujenzi Bandari ya Bagamoyo

Prof. Mbalawa, Waziri Misri wavutana, makubaliano ujenzi Bandari ya Bagamoyo

Nukta TV

Rais Samia: Nchi za Afrika zinaweza, bila ushiriki wa mataifa ya nje

Rais Samia: Nchi za Afrika zinaweza, bila ushiriki wa mataifa ya nje

Nukta TV

Mfahamu ‘African Goose’ bata mwenye kilo 14 anayeuzwa Sh2 milioni

Mfahamu ‘African Goose’ bata mwenye kilo 14 anayeuzwa Sh2 milioni

Nukta TV