Tanzania yapokea dozi milioni 1 za chanjo dhidi ya COVID-19

July 24, 2021 2:01 pm · TULINAGWE ALSON
Share
Tweet
Copy Link
  • Chanjo hiyo ni msaada kupitia mpango wa usambazaji chanjo kwa chini ya uchumi wa chini wa Covax. 
  • Balozi wa Marekani nchini Tanzania amesema ugawaji huo umelenga kuokoa maisha ya watu na kudumisha mshikamano na Tanzania na Marekani.

Dar es Salaam. Tanzania imepokea dozi zaidi ya milioni moja za chanjo dhidi ya ugonjwa wa Corona (Uviko-19) iitwayo Johnson & Johnson ikiwa ni msaada kupitia mpango wa usambazaji chanjo wa Covax ulioratibiwa na Umoja wa Afrika (AU).

Balozi wa Marekani nchini Tanzania Donald Wright amesema wametoa chanjo hizo ili kuokoa maisha ya watu lakini pia kuendeleza mshikamano na Tanzania.

“Tunatoa chanjo hizi kuokoa maisha ya watu na kulimaliza janga hili duniani. Utoaji wa chanjo hizi utakua kielelezo cha mshikamano wa miaka 60 na nchi ya Tanzania,” amesema Wright.Balozi wa Marekani nchini Tanzania Donald Wright akikabidhi chanjo katika uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere. Picha| Ubalozi wa Marekani Tanzania.

Chanjo hizo, zilizopokelewa leo mchana (Julai 24, 2021) katika Uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA),  ni sehemu ya mpango wa nchi ya Marekani kugawana na nchi mbalimbali duniani kama moja ya jitihada za kupambana na ugonjwa wa Corona duniani.

Mapokezi hayo yamefuatia maamuzi yaliyotolewa na Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan Juni 28, 2021 kuwa Tanzania iliomba kujiunga na mpango wa Umoja wa Mataifa wa upatikanaji wa chanjo wa COVAX kwa nchi za kipato cha chini. 

Jana Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Dk Dorothy Gwajima aliwaambia wanahabari Dar es Salaam kuwa mpango wa Serikali ni kutoa chanjo asilimia 60 ya watu wote nchini.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
13 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
13 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
13 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

Nukta TV

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Nukta TV

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Nukta TV