Dola ya Marekani yabaki tulivu Juni 2, 2026
- Ni baada ya kuimarika kwa asilimia 0.5 ndani ya mwezi Mei
Dar es Salaam. Dola ya Marekani imeendelea kubaki tulivu dhidi ya Shilingi ya Tanzania katika benki za CRDB na NMB baada ya kuongezeka kwa asilimia 0.5 ndani ya mwezi mmoja.
Kwa mujibu wa takwimu za viwango vya kubadilisha fedha, leo Juni 2, 2026 Dola ya Marekani imeendelea kusalia katika kiwango sawa na jana cha Sh2,585 kwa bei ya kununua na Sh2,665 kwa bei ya kuuza katika benki zote mbili.

Kutulia kwa viwango hivyo kunaashiria kuwa soko la fedha za kigeni limeendelea kuwa na utulivu kwa siku ya pili mfululizo baada ya ongezeko lililoshuhudiwa mwanzoni mwa wiki, hali inayoweza kutoa nafuu kwa wafanyabiashara na waagizaji bidhaa wanaotegemea dola katika miamala yao ya kila siku.
Kwa upande wa sarafu za kikanda, Shilingi ya Kenya na Shilingi ya Uganda zimeendelea kusalia tulivu hali inayoonyesha utulivu wa biashara na mwenendo wa fedha katika ukanda wa Afrika Mashariki