Dola ya Marekani yapaa kwa Sh5 dhidi ya Shilingi ya Tanzania Mei 19, 2026
- Ongezeko hilo ni sawa na asilimia 0.19 kwa bei ya kuuza na kununua ukilinganisha bei iliyotumika jana Mei 18, 2026 ambapo dola iliuzwa kwa Sh2,650 na kununuliwa kwa 2,570.
Dar es Salaam. Dola ya Marekani imeendelea kuimarika dhidi ya Shilingi ya Tanzania ikiongezeka thamani kwa Sh5 ndani ya siku moja kwa bei ya kuuza na kununua katika benki za kibiashara za NMB na CRDB.
Kwa mujibu wa takwimu za viwango vya kubadilisha fedha katika benki hizo mbili vinavyotumika leo Mei 19, 2026, Dola ya Marekani inauzwa kwa Sh2,655 na kununuliwa kwa Sh2,575 katika benki hizo.
Hii ni sawa na ongezeko la asilimia 0.19 kwa bei ya kuuza na kununua ukilinganisha na bei iliyotumika jana Mei 18, 2026 ambapo dola iliuzwa kwa Sh2,650 na kununuliwa kwa 2,570.

Hii inamaanisha kuwa gharama za uagizaji wa bidhaa kutoka nje kama mafuta na bidhaa nyingine muhimu zitaongezeka hali inayoweza kuchochea mfumuko wa bei na kuongeza mzigo kwa wafanyabiashara wanaoagiza bidhaa nje ya nchi.
Hali kama hiyo pia nimeonekana katika sarafu nyingine kama vile Pauni ya Uingereza, Euro pamoja na Yuani ya China huku sarafu za kikanda kama vile Shilingi ya Kenya na Uganda vikiimarika kiduchu.
Latest