Corona: Serikali ya Tanzania haijatangaza kufunga shule, vyuo

July 1, 2021 10:04 am · TULINAGWE ALSON
Share
Tweet
Copy Link
  • Baadhi ya watu wanapotoshwa kwa kusambaza habari ya mwaka jana.
  • Habari hiyo ni ya tangazo la kufunga shule na vyuo Aprili 2020.
  • Serikali haijafunga shule wala vyuo kwa sababu ya Corona.

Dar es Salaam. Kama wewe ni miongoni mwa watu waliopata video fupi kwenye mitandao ya kijamii inayosema Serikali imefunga shule na vyuo kuwakinga wanafunzi na Corona, fahamu kuwa ni uzushi. 

Licha ya kuwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wako likizo, Serikali haijatoa tamko lolote la kuzifunga shule hizo kipindi hiki.

Habari hiyo ambayo iko kwenye mfumo wa video inamuonyesha mtangazaji wa kituo cha televisheni cha ITV, Farhia Middle akitoa habari kuwa Serikali imefunga shule na vyuo kuwakinga wanafunzi na Corona.

Pia video hiyo ambayo inasambaa kwa kasi kwenye mitandao ya kijamii inamuonyesha Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitoa tangazo hilo.

“Shule zote na vyuo kuendelea kufungwa kwa tahadhari ya Corona hadi serikali itakapotoa tamko jingine,” inaeleza sehemu ya habari hiyo.

Nje, ndani ya habari hiyo

Uchunguzi uliofanywa na timu ya Nukta Fakti kwa kutumia zana za kidijitali ikiwemo TinEye umebaini kuwa taarifa hiyo ni ya kweli lakini ilitolewa na Serikali Aprili 2020 na ITV ilichapishwa katika mtandao wake wa Facebook.

Majaliwa  alitoa tamko hilo katika kikao cha kitaifa cha uratibu wa mapambano dhidi ya ugonjwa wa Corona jijini Dodoma mwaka jana na siyo mwaka huu kama inavyosambazwa na wapotoshaji.

Wanafunzi na walimu ambao shule zao zinafunguliwa kuanzia Julai 5, 2021 wametakiwa kuipuuza habari hiyo na kuendelea na maandalizi ya kuingia muhula wa pili wa masomo.

Ili kupata taarifa sahihi za Corona, Watanzania wanashauriwa kutumia vyanzo sahihi ikiwemo Wizara ya Afya na Shirika la Afya Duniani (WHO)

Pia kama Rais Samia Suluhu Hassan alivyosisitiza, wanashauriwa kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa wa Corona kwa kuvaa barakoa, kunawa mikono kwa maji tiririka na kuepuka misongamano isiyo ya lazima. 

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: HOTUBA YA BAJETI, WIZARA YA MADINI IKIWASILISHWA BUNGENI

🔴LIVE: HOTUBA YA BAJETI, WIZARA YA MADINI IKIWASILISHWA BUNGENI

Nukta TV

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Nukta Africa kuzindua Nukta AI, siku ya uhuru wa vyombo vya habari

Nukta Africa kuzindua Nukta AI, siku ya uhuru wa vyombo vya habari

Nukta TV