Corona! Nchi hizi za Afrika haziongozi kwa rushwa

July 23, 2020 6:35 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Umoja wa Mataifa umezushiwa kuwa umetangaza nchi tano zinazoongoza kwa rushwa wakati huu wa Corona.
  • Nchi ya Nigeria ndiyo kinara ikifuatiwa na nchi za Mali, Sudan, Kenya na Guinea-Bissau.
  • Habari hiyo siyo ya kweli na inalenga kupotosha. 

Dar es Salaam. Mitandao ya kijamii inaendelea kuwa nyenzo inayotumika kusambaza habari za uzushi hasa zinazohusu ugonjwa wa virusi kwa sababu ina uwezo wa kuwafikia watu wengi kwa muda mfupi. 

Nchi tano za Afrika ikiwemo Nigeria zimezushiwa kuwa ndiyo nchi zinazoongoza kwa rushwa wakati huu wa janga la Corona ambalo bado linaitesa dunia.

Habari hiyo inayodaiwa kuwa ni ya Umoja wa Mataifa (UN) iliyowekwa katika mtandao wa Twitter Julai 14, 2020, siyo ya kweli na inalenga kupotosha. 

Nchi zingine ambazo zimetajwa kuwa vinara wa rushwa wakati huu wa Corona katika habari hiyo ni Mali, Sudan, Kenya na Guinea-Bissau.


Zinazohusiana:


Ukweli ukoje

Timu ya Nukta Fakti imebaini kuwa taarifa hiyo haijatolewa na ukurasa wa Twitter wa Umoja wa Mataifa (UN).

Habari hiyo ni uzushi kwa sababu UN haijatoa tamko kama hilo katika mtandao wa Twitter wala sehemu nyingine yoyote.

Follow Us on TikTok

FOLLOW NOW

Subscribe to Our YouTube Channel

SUBSCRIBE NOW