Corona inasababishwa na virusi siyo bakteria

June 23, 2020 11:06 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Corona ni jamii ya virusi aina ya COVID-19 na siyo bakteria. 
  • Lakini baadhi ya watu ambao wanapata maradhi ya COVID-19 wanaweza kupata shida ya maambukizi ya bakteria.
  • Ukipata Corona nenda kituo cha afya ufanyiwe uchunguzi.

Dar es Salaam. Ugonjwa wa virusi vya Corona ni zaidi ya ugonjwa unaothiri afya za watu kwa sasa baada ya kuwa ni chanzo cha uzalishaji wa habari za uzushi ambazo zina madhara zaidi kwa uchumi na maisha ya watu. 

Kwa sasa, mkanganyiko ambao umekuwa ukitokea hasa kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii ni kuhusu kisababishi cha ugonjwa wa Corona.

Wapo wanaosema unasababishwa na virusi na wengine wanadai ni bakteria. Licha ya kuwepo elimu ya muda mrefu kuhusu corona, bado kuna maudhui potofu kuhusu chanzo cha maradhi yanajipenyeza. Je, nani yuko sahihi?


Zinazohusiana:


Ukweli uko hivi

Shirika la Afya Duniani (WHO) linaeleza kuwa Corona inasababishwa na kirusi aina ya COVID-19 na siyo bakteria kama inavyodhaniwa na kuelezwa na baadhi ya watu mtandaoni. 

“Kirusi kinachosababisha COVID-19 ni familia ya virusi vinavyojulikana kama “Coronaviridae”, imesema WHO.

WHO imeeleza kuwa dawa za kuzuia au kuua bakteria (Antibiotics) haziwezi kufanya kazi dhidi ya virusi hivyo kwa sababu matibabu yake hutegemea dalili za mgonjwa. 

Hata hivyo, baadhi ya watu ambao wanapata maradhi ya COVID-19 wanaweza kupata shida ya maambukizi ya bakteria.

“Kwa kesi hii, dawa ya antibiotics zinaweza kupendekezwa na mtoaji huduma za afya,” imesema WHO. 

 Shirika hilo limeendelea kusisitiza kuwa mpaka sasa hakuna dawa iliyothibitishwa kutibu COVID-19.

Kama umepata dalili za ugonjwa huo nenda katika kituo cha afya ili upate matibabu stahiki.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
16 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
16 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Nukta TV

Rais Samia: Kalamu yangu ina hatari, sijawahi kusaini mtu kunyongwa

Rais Samia: Kalamu yangu ina hatari, sijawahi kusaini mtu kunyongwa

Nukta TV

Rais Samia: Matumizi jina Samia, likiwa kila mahali inachosha, tafuteni wengine

Rais Samia: Matumizi jina Samia, likiwa kila mahali inachosha, tafuteni wengine

Nukta TV