Chanjo ya Uviko-19 Afrika Mashariki bado ngoma ngumu
- Tanzania yawa kinara kwa kuchanja watu wengi.
- Kongo DRC, Burundi na Sudani kusini zasua sua.
Dar es salaam. Janga la Uviko-19 bado limeendelea kuitesa dunia licha ya juhudi mbalimbali kukabiliana nalo.
Shirika la Afya Duniani (WHO) limeeleza kuwa hivi sasa jumla ya visa milioni 600.3 vya maambukizi ya Uviko-19 na vifo milioni 6.4 vimeripotiwa duniani kote.
Wakati bara la Afrika likifikisha jumla ya maambukizi milioni 9.2 bado juhudi za kutoa chanjo hazijawa za dhati katika baadhi ya mataifa yakiwemo ya ukanda wa Afrika Mashariki.
Kwa mujibu wa data zilizochapishwa na WHO hadi Septemba 6 mwaka huu, Tanzania ndio nchi iliyokuwa imechanja watu wengi zaidi kulinganisha na nchi nyingine za ukanda huo ambapo jumla ya watu milioni 17.3 wamechanjwa.

Latest
