5G inasambaza corona? Hapana, ni uzushi
- Virusi vya ugonjwa wa corona (COVID-19) haviwezi kusambaa kupitia mawimbi ya redio au mfumo wowote wa mawasiliano ya simu.
Dar es Salaam. Kumekuwa na habari zinasambaa kwa kasi mtandaoni kuwa teknolojia mpya ya mawasiliano ya 5G inasambaza virusi vya corona, hata hivyo, taarifa hizo hazina ukweli wowote kisayansi.
Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) virusi vya ugonjwa wa corona (COVID-19) haviwezi kusambaa kupitia mawimbi ya redio au mfumo wowote wa mawasiliano ya simu.
Ikumbukwe ugonjwa huo unasambaa kwa kasi hata kwenye mataifa ambayo hayana teknolojia hiyo ya 5G.
“COVID-19 inasambazwa kupitia majimaji ya mtu anapopiga chafya, kukohoa au kuzungumza. Watu wanaweza pia kuambukizwa virusi hivyo kwa kugusa maeneo yenye virusi halafu baadaye wakagusa pua, macho na midomo yao,” WHO inaeleza.
Latest