Hapana: Huwezi kuambukizwa Corona kwa dalili zinazoonekana pekee
- Wapo watu wanaopata ugonjwa huo pasipo kuonyesha dalili zozote.
- Upimaji ndiyo njia inayoweza kukufahamisha kama una ugonjwa huo au la!
- Zingatia miongozo ya yote afya ikiwemo kuvaa barakoa na kunawa mikono.
Dar es Salaam. Wakati janga la Corona likiendelea kuitesa dunia, wapo baadhi ya watu wanaaamini kuwa ugonjwa huo unasambazwa kwa dalili zinazoonekana tu na wale wasioonyesha dalili zozote hawawezi kupata maambukizi ya ugonjwa huo.
Dalili zilizozoeleka kwa watu wanaopata ugonjwa huo aina ya COVID-19 ni pamoja na kikohozi, homa, kupumua kwa shida, maumivu ya misuli na koo, kushindwa kutambua harufu na ladha ya chakula na vitu.
Hata hivyo, ni muhimu kufahamu kuwa mtu asipoonyesha dalili hizo, siyo kwamba hana COVID-19.
Kwa mujibu wa kituo cha afya cha BeyHealth cha nchini Marekani, asilimia 80 ya watu wanaoambukizwa ugonjwa huo hawaonyeshi dalili zozote na wanaweza kuendelea kuwaambukiza watu walio karibu yao wakiwemo wanafamilia na marafiki pasipo kujua.
“Watu wenye COVID-19 wameripoti kuonyesha dalili mbalimbali zisizoonekana na zile zinazoonekana,” kinaeleza kituo hicho ambacho kinamiliki mfumo wa matibabu wa mtandaoni.
Zinazohusiana:
- Mikakati ya Tanzania kukabiliana na virusi vya Corona
- Picha, sauti ya uzushi virusi vya corona zinavyojipenyeza mtandaoni Tanzania
- Unayotakiwa kufahamu kuhusu virusi vya Corona
Dalili zingine za ugonjwa huo ambazo hazijaripotiwa sana lakini zimekuwa zikitokea kwa watu ni pamoja na kichefu chefu, kutapika na kuharisha.
Tunakumbushwa kuendelea kujikinga na ugonjwa huo kwa kufuata ushauri unaotolewa na wataalam wa afya ikiwemo kuvaa barakoa na kutumia tishu wakati wa kukohoa au kupiga chafya.
Latest
