Rais Samia kuunda kamati ya wataalamu kuhusu Corona Tanzania

April 6, 2021 9:14 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Kamati ya wataalamu itachunguza kwa undani suala la ugonjwa wa homa ya mapafu unaosababishwa na virusi vya Corona (Covid-19).
  • Itatoa mapendekezo kwa Serikali namna ya kulishughulikia suala hilo. 

Dar es Salaam. Rais Samia Suluhu Hassan amesema anakusudia kuunda kamati ya wataalamu wachunguze kwa undani suala la ugonjwa wa homa ya mapafu unaosababishwa na virusi vya Corona (Covid-19) ili iishauri Serikali hatua madhubuti za kuchukua.

Rais Samia ameeleza leo Aprili 6, 2021 baada ya kuwaapishwa makatibu wakuu, naibu makatibu wakuu na wakuu wa taasisi za umma na kusema Tanzania siyo kisiwa.

“Kuhusu suala la Covid nakusudia niunde kamati ya wataalamu waliangalie suala la Covid-19 kwa upana wake. Waangalie remedies (suluhu) wanazosema zitatusaidia kwa upana wake kitaalamu kabisa halafu watushauri Serikali,”

“Halifai kulinyamazia. Aidha kulikataa au kulikubali bila kufanya utafiti kitaalamu. Tutafanya tafiti za kitaalamu. Tutaunda kamati ya kitaalamu. Watuambie upeo wa swali au tatizo hili lilivyo na hayo yanayopendekezwa na ulimwengu kuja kwetu,” amesema Rais Samia.


Soma zaidi:


Kamati hiyo, kwa mujibu wa Rais, itasaidia kubaini ukweli wa jambo hilo kwa kutumia wataalamu wa ndani.

“Hatuwezi kujitenga kama kisiwa na hatuwezi tu kupokea yanayoletwa kwetu bila kufanya utafiti wa kwetu. Rais (Jakaya) Kikwetea aliwahi kutuambia “Akili za kuambiwa? Changanya na zako” kwa hiyo tuweke na zetu tuwe na msimamo maalum unaoeleweka. Siyo tunasoma mambo ya Covid ulimwenguni, Tanznaia desh, desh, haieleweki. Tueleweke kama tunakubali, tunakataa. Tunafanyaje. Tueleweke,” amesema kiongozi huyo wa juu zaidi nchini.

Kauli hiyo ya Rais Samia ni ya kwanza kutolewa kuhusu masuala ya Covid-19 tangu alipoingia madarakani Machi 19 kufuatia kifo cha Hayati Rais John Magufuli kilichotokea Machi 17 mwaka huu. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
25 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
26 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
26 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Nukta TV

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Nukta TV

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Nukta TV