Hatua za kuwasaidia walemavu kujikinga dhidi ya Uviko-19
Dar es Salaam. Takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO) zinaonyesha kuwa zaidi ya watu bilioni 1 duniani sawa na asilimia 15 wanaishi na ulemavu, huku nusu ya idadi hiyo ikikumbana na changamoto mbalimbali za huduma za afya.
Kutokana na hatari ya janga la Uviko-19, ni muhimu kwa Serikali na jamii kwa ujumla kuchukua hatua mbalimbali za kusaidia walemavu ili waweze kujikinga dhidi ya janga hilo.
Hatua hizo ni pamoja na kuhakikisha urahisi wa kupima na kuchanja chanjo ya Uviko-19 kwa walemavu, vilevile kutoa misaada kwa familia zenye walemavu ambazo zina kipato duni.
Kujifunza zaidi tazama infografia hii:

Latest
