Umuhimu wa chanjo ya Uviko-19 kwa walemavu
Dar es salaam. Kutokana na  changamoto mbalimbali wanazopitia walemavu, zinawaweka katika hatari kubwa ya kuambukizwa ugonjwa wa Corona (Uviko-19) ni muhimu kuwapa kipaumbele katika utoaji wa chanjo ya ugonjwa huo.
Changamoto hizo ni pamoja na  ugumu wa kupata taarifa kuhusu Uviko-19 hasa kwa walemavu wa macho na masikio.
Vile vile ugumu wa kujitenga na watu wengine hasa kwa walemavu wanaoishi katika uwingi wa watu na wale ambao wanaihitaji wasaidizi.
