Hali ya Uviko-19 Tanzania

November 30, 2021 7:59 am · Herimina
Share
Tweet
Copy Link
  • Maambukizi ya ugonjwa huo yafikia 26,261 huku vifo vikiwa 730.
  • Wananchi wasisitizwa kuzingatia maelekezo ya kiafya kujikinga na Uviko-19.

Dar es Salaam. Hadi kufikia Novemba 19, 2021, Tanzania ilikuwa imeripoti visa vya ugonjwa wa Corona 26,261 na vifo 730.

Kutokana  na mwenendo wa Uviko-19 duniani, ambao hadi Novemba 29, 2021 umeshasababisha zaidi ya vifo milioni 5.2 duniani, Wizara ya Afya nchini imeendela kuwasihi wananchi kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa huo ikiwemo kupata chanjo ya Uviko-19, kuvaa barakoa wakati wote pamoja na kunawa mikono kwa sabuni na maji tiririka.

Vilevile, Serikali inaendelea kufuatilia mwenendo wa  aina ya kirusi kipya cha Uviko-19 cha ‘Omicron’ na kufanya tathmini ya hatua madhubuti za kuchukua ili kukabiliana na wimbi la nne la Uviko-19.

Follow Us on TikTok

FOLLOW NOW

Subscribe to Our YouTube Channel

SUBSCRIBE NOW