Hali ya Uviko-19 Tanzania
- Maambukizi ya ugonjwa huo yafikia 26,261 huku vifo vikiwa 730.
- Wananchi wasisitizwa kuzingatia maelekezo ya kiafya kujikinga na Uviko-19.
Dar es Salaam. Hadi kufikia Novemba 19, 2021, Tanzania ilikuwa imeripoti visa vya ugonjwa wa Corona 26,261 na vifo 730.
Kutokana na mwenendo wa Uviko-19 duniani, ambao hadi Novemba 29, 2021 umeshasababisha zaidi ya vifo milioni 5.2 duniani, Wizara ya Afya nchini imeendela kuwasihi wananchi kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa huo ikiwemo kupata chanjo ya Uviko-19, kuvaa barakoa wakati wote pamoja na kunawa mikono kwa sabuni na maji tiririka.
Vilevile, Serikali inaendelea kufuatilia mwenendo wa aina ya kirusi kipya cha Uviko-19 cha ‘Omicron’ na kufanya tathmini ya hatua madhubuti za kuchukua ili kukabiliana na wimbi la nne la Uviko-19.

Latest