Corona ipo, chukua tahadhari

June 8, 2022 8:38 am · admin
Share
Tweet
Copy Link
  • Kati ya Mei 5 hadi Juni 3, Wizara hiyo imeripoti jumla ya visa vipya 160.

Dar es Salaam. Wizara ya Afya nchini Tanzania imewataka Watanzania kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya maambukizi ya Uviko-19 ikiwemo kupata chanjo kwa sababu ugonjwa huo bado upo.

Kati ya Mei 5 hadi Juni 3, Wizara hiyo imeripoti jumla ya visa vipya 160 ingawa hakujaripotiwa kifo chochote katika miezi miwili iliyopita.

Tarifa hiyo ya wizara hiyo iliyotolewa Juni 7, 2022 imeainisha mikoa ambayo imeripoti kiwango kikubwa cha maambukizi ambapo Dar es salaam imeripoti visa 130, Arusha (10), Mwanza (5), Shinyanga (4), Mtwara (3), Dodoma (2) na Mara  ni visa viwili.

Waliopata chanjo kati ya Mei 5 mpaka Juni 3 ni 775,680 huku wagonjwa watatu waliothibitika kuwa na maabukizi na kulazwa wote walikuwa hawajapata chanjo hivyo wizara imeendelea kusisitiza wananchi kupata chanjo kamili ya Uviko-19.

Kujikinga na ugonjwa huo, wananchi wametakiwa kupata chanjo, kunawa mikono mara kwa mara, kuvaa barakoa na kuepuka mikusanyiko isiyo ya lazima. 

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: LIVE:WABUNGE WAKIWACHAPA MASWALI MAWAZIRI | Bunge la 13 | Kikao cha 28

🔴LIVE: LIVE:WABUNGE WAKIWACHAPA MASWALI MAWAZIRI | Bunge la 13 | Kikao cha 28

Nukta TV

Top 10 ya magari yanayotumia kiwango kidogo cha mafuta

Top 10 ya magari yanayotumia kiwango kidogo cha mafuta

Nukta TV

SGR yaingizia Serikali Sh169.37 bilioni tangu kuanza kwa safari Juni 2024

SGR yaingizia Serikali Sh169.37 bilioni tangu kuanza kwa safari Juni 2024

Nukta TV