Tahadhari: Kirusi kipya cha Corona

November 29, 2021 12:10 pm · Herimina
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni kirusi cha Omicron, chenye uwezo wa kusambaa haraka.
  • Wananchi watakiwa kuendelea kuchukua tahadhari.

Dar es salaam. Shirika la Afya Duniani (WHO), Novemba 26, 2021 liliripoti uwepo wa aina mpya ya kirusi cha Uviko-19 kiitwacho “Omicron”, kinachosemekana kuwa na uwezo wa kusambaa haraka.

Kutokana na hali hiyo, Wizara ya Afya Tanzania imetoa tahadhari kwa Watanzania kuendelea kufuata ushauri wa wataalam wa afya kujikinga na maambukizi ya ugonjwa huo.

Hatua hizo ni pamoja na kuchanja chanjo ya Uviko-19 ambazo zinatolewa bure kwenye vituo vya afya na kuepuka sehemu zenye mikusanyiko ya watu.

Vile vile, uvaaji barakoa, kunawa mikono na sabuni kwa maji tiririka.

Follow Us on TikTok

FOLLOW NOW

Subscribe to Our YouTube Channel

SUBSCRIBE NOW