Corona bado ipo Tanzania, chukua tahadhari
Dar es Salaam. Wizara wa Afya imesema hadi kufika Februari 6, 2022 jumla ya watu 33,482 wamethibitika kuwa na maambukizi ya Corona (Uviko-19) na 792 kati yao wamepoteza maisha huku Serikali ikiimarisha mapambano dhidi ya ugonjwa huo.

Hata hivyo, amesema mwenendo wa utoaji wa chanjo ni wa kuridhisha ambapo takwimu za Februari 6, 2022 jumla ya watu milioni 2.11 milioni sawa na asilimia 3.6 ya Watanzania waliokuwa wamepata chanjo kamili.
