Tanzania yapokea shehena nyingine ya chanjo ya Uviko-19

January 26, 2022 10:55 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link

Dar es Salaam. Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu amesema hadi kufika Januari 23, 2022 jumla ya watu 33,000 wamethibitika kuwa na maambukizi ya Corona (Uviko-19) na 781 kati yao wamepoteza maisha  huku Serikali ikiimarisha mapambano dhidi ya ugonjwa huo.

Ummy aliyekuwa akizungumza leo Januari 26, 2022 jijini Dar es Salaam wakati wa mapokezi ya chanjo aina ya Sinopharm kwa ufadhili wa Serikali ya China jumla ya dozi 800,000 ambazo zitatumika kuchanja wananchi 400,000 amesema watu wanapaswa kuendelea kuchukua tahadhari.

“Naishukuru Serikali ya China kwa kuwezesha upatikanaji wa chanjo hizi awamu ya pili kwa chanjo za aina hii awamu ya kwanza tulipokea jumla ya dozi 500,00 ambazo zilitumika kuchanja watu 250,000,” aamesema Ummy.

Hata hivyo, amesema mwenendo wa utoaji wa chanjo ni wa kuridhisha ambapo takwimu za Januari 25, 2022 jumla ya watu milioni 1,9 milioni sawa na asilimia 3.33 ya Watanzania waliokuwa wamepata chanjo kamili.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
26 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
26 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
26 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Nukta TV

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Nukta TV

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Nukta TV