Infografia: Ukaribu wa viongozi na wananchi bado changamoto Maswa
Dar es Salaam. Utafiti wa awali wa ngazi ya kaya wilayani Maswa mkoani Simiyu (Machi 12 – 14 Aprili 2021), uliofanywa na Shirika la Twaweza unaonyesha kuwa wananchi na viongozi katika wilaya hiyo wanakutana mara chache kuzungumza kuhusu maendeleo.
Kwa mujibu wa utafiti huo ni wakazi 3 kati ya 10 ndiyo wamewahi kukutana na kuzungumza na mwenyekiti wa kijiji, huku hali mbaya ikiwa ni kwa mbunge ambapo asilimia 2 pekee ya wakazi wilayani humo wameonana na mbunge wao walau mara moja.
Mara ya mwisho kukutaa na kiongozi wako ilikuwa lini?
