Lindi yafunika bei ya viazi mviringo

January 31, 2022 12:23 pm · Wilson
Share
Tweet
Copy Link
  • Gunia la kilo 100 la viazi mviringo katika masoko ya Lindi linauzwa kwa Sh120,000.
  •  Bei ndiyo bei ya juu kabisa Tanzania Bara.
  • Bei ya chini ya zao hilo ni Sh46,000 inayotumika mkoani Njombe.

Dar es Salaam. Watumiaji wa viazi mviringo hasa kutengeneza chipsi katika Mkoa wa Lindi leo watalala na maumivu kutokana na bei ya jumla ya zao hilo  kuuzwa kwa bei ya juu kuliko maeneo mengine Tanzania Bara. 

Takwimu za mazao makuu ya chakula zilizotolewa na Wizara ya Viwanda na Biashara  leo (Januari 31, 2022) zinaeleza kuwa gunia la kilo 100 la viazi mviringo katika masoko ya Lindi linauzwa kwa Sh120,000.

Bei hiyo ni mara mbili zaidi ya bei inayotumika katika  masoko ya Njombe ambayo ni Sh46,000, jambo linalowanufaisha  zaidi wafanyabiashara ambao wamepeleka bidhaa hiyo mkoani humo. 

Bei hiyo inayotumika Lindi ndiyo bei ya juu Zaidi huku ya Njombe ikiwa ni ya chini ikilinganishwa na bei zinazotumika katika maeneo mengine nchini.

Viazi mviringo ni miongoni mwa mazao makuu ya chakula ambavyo vimekuwa vikitumiwa kwa matumizi mbalimbali ikiwemo kukaanga chipsi ambazo zinapendwa zaidi na mabachela.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Nukta TV

Rais Samia: Kalamu yangu ina hatari, sijawahi kusaini mtu kunyongwa

Rais Samia: Kalamu yangu ina hatari, sijawahi kusaini mtu kunyongwa

Nukta TV

Rais Samia: Matumizi jina Samia, likiwa kila mahali inachosha, tafuteni wengine

Rais Samia: Matumizi jina Samia, likiwa kila mahali inachosha, tafuteni wengine

Nukta TV