Youtube yawaongezea nguvu wanamitindo duniani

September 6, 2019 11:13 am · TULINAGWE ALSON
Share
Tweet
Copy Link
  • Imeongeza kipengele kipya kwa ajili ya mitindo baada ya kubaini kuwa ina wafuasi wengi. 
  • Kitasaidia kuongeza mapato na ukuaji wa tasnia hiyo duniani.

Mtandao wa Youtube ambao uko chini ya kampuni ya Google umeamua kuipa kipaumbele tasnia ya mitindo baada ya kuanzisha kipengele kimpya kwa ajili shughuli hizo.

Mabadiliko hayo yamefanyika kufuatia tafiti iliyofanywa na mtandao huo na kubaini kuwa watumiaji wengi katika mtandao wana chaneli zenye maudhui hasa ya yanayohusu mitindo, mavazi na urembo. 

Kipengele hicho kinadhihirisha wazi kuwa Youtube imekusudia kuboresha huduma zake na kukidhi mahitaji ya watu wanaotembelea mtandao huo kila siku. 

Kwa mujibu wa Youtube, maudhui ya mitindo na usanifu wa mavaziyameongezeka zaidi ya mara sita kati ya mwaka 2014 na 2018, jambo linatoa fursa kwao kuweka msisitizo katika tasnia hiyo inayoajiri watu wengi duniani.


Zinazohusiana:


Mabadiko hayo yamefanyika wiki hii kwa Youtube kuonyesha shughuli mbalimbali za mitindo ikiwemo matamasha ya mitindo na mavazi yanayofanyika maeneo mbalimbali duniani ili kuwarahisishia watu kuyaona wakiwa popote duniani. 

Youtube inaamini kuwa kipengele hicho kitachagiza ukuaji wa tasnia ya fasheni duniani na kuongeza mapato ya mtandao huo na watu waliowekeza katika shughuli hizo.

Youtube kutambua mchango wa wanamitido duniani. Picha| Mtandao.

Follow Us on TikTok

Subscribe to Our YouTube Channel

Subscribe

Loading videos...

Loading videos...

Loading videos...