WHO sasa yaingia Whatsapp kutoa taarifa za Corona

March 23, 2020 9:59 am · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link

Watu wenye uhitaji wa kuzipata ambapo watatakiwa kujiunga kwa kutumia kiunganishi hiki shorturl.at/nQY23 au kwa kutuma neno “hi” kwa namba hii +41 79 893 18 92 kwa WhatsApp. Picha|Wired.


  • Shirika hilo limeshirikiana na Whatsapp na Facebook kutoa huduma ya meseji za WhatsApp.
  • Taarifa hizo ni pamoja na zile za watu wanaoambukizwa, kufariki na jinsi ya kujikinga na ugonjwa huo hatari. 

Dar es Salaam. Shirika la Afya Duniani (WHO) limezindua huduma ya ujumbe mfupi wa maneno (meseji) kwa kushirikiana na mitandao ya kijamii ya WhatsApp na Facebook ili kuwalinda watu dhidi ya ugonjwa wa virusi vya Corona. 

Huduma hiyo iliyozinduliwa jana (Machi 20, 2020) inalenga kuwafikia watu bilioni 2 na kuwawezesha kupata taarifa sahihi za Corona moja kwa moja katika simu zao kupitia mtandao wa WhatsApp.

“Kutoka kwa viongozi wa Serikali hadi kwa wafanyakazi wa afya, familia na marafiki, huduma hii ya meseji itawapatia habari za papo kwa papo na taarifa muhimu za virusi vya Corona ikiwemo undani wa dalili na jinsi watu wanaweza kujikinga wao na wengine,” inaeleza taarifa ya WHO.

Pia huduma hiyo inatoa taarifa za hali halisi ya ugonjwa ikiwemo idadi ya watu wanaoambukizwa, kufariki kila siku na kuzisaidia Serikali na watoa maamuzi kuwakinga watu wao.


Zinazohusiana:


WHO imesema taarifa hizo zitawafikia tu watu wenye uhitaji wa kuzipata ambapo watatakiwa kujiunga kwa kutumia kiunganishi hiki shorturl.at/nQY23 au kwa kutuma neno “hi” kwa namba hii +41 79 893 18 92 kwa WhatsApp. 

Baada ya hapo utaanza kupokea taarifa zote za Corona katika kiganja chako zitakazokusaidia kufanya maamuzi sahihi ya kujikinga na ugonjwa huo.

Mfumo huo wa meseji umetengenezwa na WHO kwa kushirikiana na taasisi ya Praekelt.Org kwa kutumia teknolojia ya  “Turn” (mashine inayotumia kompyuta kusoma tabia za watu).

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
25 Aug, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
25 Aug, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
25 Aug, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Elimu ya kodi mwarobaini wa wafanyabiashara kuikwepa TRA, ianzie shuleni

Elimu ya kodi mwarobaini wa wafanyabiashara kuikwepa TRA, ianzie shuleni

Nukta TV

Rais Samia: Serikali chini ya Magufuli haikutaka kuyumbishwa kukamili kwa JNHPP

Rais Samia: Serikali chini ya Magufuli haikutaka kuyumbishwa kukamili kwa JNHPP

Nukta TV

Rais Samia: Umeme wa SGR hautoingiliwa, Dodoma umeme uhakika 24/7

Rais Samia: Umeme wa SGR hautoingiliwa, Dodoma umeme uhakika 24/7

Nukta TV