Wanafunzi vyuo vya kati Tanzania kupewa mikopo 2023-24
- Fani za sayansi, afya, elimu pamoja na ufundi kupewa kipaumbele.
- Kuanza kutekelezwa Julai 2023 kwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza.
- Ni kufuatia mabadiliko sera ya elimu ya mwaka 2014 toleo la mwaka 2023.
Dar es Salaam. Serikali ya Tanzania imependekeza kuwapa mikopo wanafunzi watakaochaguliwa kujiunga na vyuo vya kati ambao watakaosoma fani za kipaumbele kama vile sayansi, afya pamoja na elimu kuanzia Julai 2023.
Waziri wa Fedha na Mipango Mwigulu Nchemba aliyeukuwa akisoma hotuba ya Najeti Kuu ya Serikali bungeni jijini Dodoma amewaambia wabunge kuwa mapendekezo hayo ni kutokana na mabadiliko sera ya elimu ya mwaka 2014 toleo la mwaka 2023.
“Serikali inalenga kutoa elimu ya amali kwa ngazi zote kuanzia shule za awali, elimu ambayo inamwezesha kijana wa kitanzania kujiajiri au kuajiriwa na hivyo kutoa mchango mkubwa kwenye uchumi wa taifa hili,” amesema Dk. Nchemba.
Hata hivyo Waziri Nchemba ameongeza kuwa kuanzishwa kwa programu hiyo ya mikopo itawalenga wanafunzi waliochaguliwa na Serikali kusoma kwenye vyuo vya kati vya elimu katika fani za kipaumbele ambazo ni sayansi elimu afya ufundi na elimu.
Soma zaidi;
- Serikali yapendekeza kuondoa ada vyuo vya ufundi Tanzania
-
Pato la mtu Tanzania laongezeka kwa zaidi ya Sh135,000 mwaka 2022
- Deni la Serikali Tanzania laongezeka hadi Sh79.1 trilioni
Hatua hiyo itaanza kwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza watakao chaguliwa kujiunga katika vyuo kati kwa mwaka mpya wa fedha 2023/24
Aidha hatua hii inakuwa ni miongoni mwa mabadiliko ya mtaala katika sekta ya elimu yanayofanywa na Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan.
Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia inakusudia kukamilisha mabadiliko ya Sheria ya Elimu pamoja na kuanza utekelezaji wa mitaala mipya kwa ngazi zote kuanzia Julai 2023.
Latest
