Zifahamu kozi sita zitazopewa kipaumbele mkopo wa HESLB ngazi ya Diploma 2023 – 24

October 4, 2023 1:05 pm · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni pamoja na kozi za afya na sayansi shirikishi.
  • Serikali yasema hatua hiyo itaongeza wataalamu nchini.
  • Wanafunzi watakiwa kuchangamkia fursa na kusoma kwa bidii.

Dar es Salaam. Serikali imezindua mwongozo wa utoaji mikopo katika ngazi ya diploma unaotarajiwa kunufaisha wanafunzi 8,000 nchini huku kipaumbele kikiwekwa katika kozi sita ikiwemo fani ya afya na sayansi.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Adolf Mkenda aliyekuwa akizungumza wakati wa uzinduzi wa mwongozo huo leo Oktoba 4, 2023, amesema Sh48 bilioni zimetengwa kufanikisha utoaji wa mikopo hiyo.

“Ni vizuri kabla hujaomba kaangalie, usiseme tu ni maeneo ya afya, tumenyumbulisha na kuanisha maeneo yenye uhitaji mkubwa zaidi ambayo mara nyingi Serikali ikitaka kuajiri watu haiwapati,” amesema Mkenda jijini Dar es Salaam.


Bofya hapa kusoma muongozo wa utoaji mikopo kwa ngazi ya diploma mwaka 2022/2023 


Kozi nyingine zilizopewa kipaumbele katika utoaji wa mikopo hiyo ni ualimu wa Sayansi, Hisabati na  Mafunzo ya  Amali, Usafiri na usafirishaji, Uhandisi na nishati, Madini na sayansi ya ardhi pamoja na Kozi ya kilimo na mifugo.

Kuzinduliwa kwa mwongozo huo kutawafuta machozi mamia ya wanafunzi wa vyuo vya kati waliokuwa wanashindwa kuendelea na masomo hayo kutokana na gharama za masomo katika ngazi hiyo kuwa juu.

Uamuzi wa Serikali kutoa mikopo kwa vyuo vya kati Tanzania uliotangazwa wakati wa bajeti ya mwaka 2023/24  ni miongoni mwa taarifa zilizopokelewa kwa shangwe na mamilioni ya Watanzania.

Katika hatua nyingine, Profesa Mkenda amesema utoaji wa mikopo hiyo kwa wanafunzi watakaosoma kozi hizo kutaongeza upatikanaji wa wataalamu waliobobea katika taaluma hizo zenye umuhimu nchini.

“Serikali imejenga hospitali, zahanati na vituo vya afya nchini kote ambavyo vinahitaji wataalamu, nasisi tumeambiwa mfano kupata wataalamu wa  clinical dentist( daktari wa meno) ni kazi kubwa sana…

…Ni wataalamu tunawahitaji lakini kila mara hata Serikali ikitaka kuwaajiri inapata shida kuwapata,” ameongeza Mkenda.

Kwa upande wake rais wa Shirikisho la Wanafunzi wa Elimu ya Juu Tanzania (Tahliso) Maria John, amewataka wanafunzi wa vyuo vya kati kuchangamkia fursa ya kuomba mikopo hiyo, huku wakisoma kwa bidii ili kuiwezesha Serikali kunufaika na mikopo waliyoitoa.


Soma zaidi:CAG aibua madudu zaidi bodi ya mikopo elimu ya juu Tanzania


“Unakuta wengine wakishapata hiyo mikopo hawasomi, wanalala tu au hawaingii darasani, wanafunzi wenzangu msifanye hivyo kwa sababu mwisho wa siku mtafeli na mkifeli mnajua hamuwezi kupata tena mkopo,” amesema.

Dirisha la maombi ya mikopo kwa vyuo vya kati litakuwa wazi kwa siku 15 kuanzia tarehe saba mpaka tarehe 22 mwezi huu, ambapo maombi yote yanatakiwa kutumwa kwa  nakala laini (soft copy) kupitia tovuti ya bodi ya mikopo 

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.