Uviko-19: Kutopata mabadiliko baada ya kuchanjwa haimaanishi umepata chanjo feki

October 7, 2022 11:59 am · admin
Share
Tweet
Copy Link
  • Wataalamu wasisitiza mabadiliko hutokea kwa namna tofauti kulingana na mhusika.

Dar es salaam. Chanjo ya Uviko-19 inaendelea kutolewa na mataifa mbalimbali duniani kama njia mojawapo ya kupambana na ugonjwa huo ambao umeathiri pakubwa shughuli za kijamii na kiuchumi duniani.

Siku za hivi karibuni kumeripotiwa kuwepo kwa uzushi kuwa wale ambao hawakupata mabadiliko ya kimwili mara baada ya kupata chanjo basi hawakuchanjwa chanjo halisi ya Uviko-19 bali ‘placebo’.

WHO kanda ya Afrika  katika taarifa yake iliyochapishwa Septemba 29 kwa mfumo wa video katika mtandao wa Twitter imekanusha uzushi huo na kueleza kuwa ‘placebo’ hutumika tu wakati wa majaribio ya dawa au chanjo na hufanyika maabara pekee.


Soma zaidi:


Placebo ni nini

WHO imeeleza kuwa placebo ni dutu ambazo hutumika wakati wa kufanya majaribio ya dawa maabara. Husajiliwa na kufanana na dawa lakini hazina kemikali hai ndani yake.

“Dutu hizi hutumika maabara pekee chini ya uangalizi maalum na haziruhusiwi kutumika nje ya maabara,” inafafanua sehemu ya taarifa ya WHO.

Kutopata mabadiliko ya kimwili mara baada ya kupokea chanjo ya Uviko-19 haimaanishi kuwa umepokea chanjo feki au chanjo haifanyi kazi bali mabadiliko yanakuwa yanatokea katika namna nyingine.

Kwa mujibu wa Shirika la Afya ulimwenguni WHO hadi Octoba 6,2022 jumla ya chanjo bilioni 12.7 zimetolewa duniani kote huku watu bilioni 5.3 wakipata angalau dozi moja ya chanjo na watu bilioni 4.9 wakipata dozi kamili ya chanjo.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
7 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
7 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

Nukta TV

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Nukta TV

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

Nukta TV