Hapana: Chanjo ya Uviko-19 haibadilishi hedhi kwa wanawake

October 6, 2022 7:46 am · admin
Share
Tweet
Copy Link
  • Wataalamu wa afya wasema ni uzushi unaolenga kuzuia watu kupata chanjo.
  • Wafafanua hakuna chanjo ya Uviko-19 inayoweza kutoka nje ya mwili.

Dar es salaam. Juhudi  za kukabiliana na janga la Uviko-19 zinaendelea ambapo pamoja na njia nyingine kama kuvaa barakoa na kunawa mikono kupata chanjo ya Uviko-19 inatajwa kama ndiyo njia salama zaidi ya kujikinga na ugonjwa huo.

Pamoja na wataalamu wa afya kuthibitisha kuwa chanjo za Uviko-19 ni salama na hazina madhara kwa afya ya binadamu bado kumekuwepo na habari potofu ambazo zimekuwa zikitolewa kwenye jamii kuhusu chanjo.

Uzushi wa hivi karibuni ni ule unaodai kuwa mwanamke ambaye hajapata chanjo anapokuwa karibu na wanawake waliopata chanjo basi mzunguko wake wa hedhi unaweza kuathirika.

Wataalamu kutoka Shirika la Afya Duniani (WHO) wamekanusha uzushi huo kwa kufafanua kuwa kitaalamu jambo hilo huitwa ‘Vaccine shedding’ ambapo sehemu ya chanjo hutolewa ndani au nje ya mwili ikiwa tu ilikuwa na sehemu dhaifu ya virusi.

“Hakuna chanjo ya Uviko-19 iliyoidhinishwa ambayo ina sehemu ya virusi kwa hiyo watu waliochanja hawawezi kutoa virusi vya Corona kupitia chanjo,” inasomeka sehemu ya taarifa hiyo iliyotolewa Septemba 27 mwaka huu.


Soma Zaidi


WHO imesisitiza kuwa kwa namna yoyote ile kuwa karibu na mtu aliyepata chanjo hakuwezi kuathiri mzunguko wa hedhi wa mwanamke hivyo wamewataka watu kupuuza madai hayo yenye lengo la kukwamisha juhudi za utoaji wa chanjo.

Itakumbukwa kuwa ni miaka mitatu sasa imepita tangu ugonjwa wa Uviko-19 uibuke huku tiba kamili ikiwa haijapatikana na chanjo imetajwa kama njia pekee iliyothibitishwa  kuwa na uwezo wa kukinga watu na ugonjwa huo unaoathiri mapafu.

Kwa mujibu wa WHO mpaka kufikia Septemba 27 mwaka huu jumla ya dozi bilioni 12.6 za chanjo zilikuwa zimetolewa duniani kote ambapo Tanzania mpaka sasa watu milioni 18.8 wamepata dozi kamili ya chanjo ya Uviko-19.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
16 Aug, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
17 Aug, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
17 Aug, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Rais Samia: AFCON ni fursa, wawekezaji karibuni kuwekeza

Rais Samia: AFCON ni fursa, wawekezaji karibuni kuwekeza

Nukta TV

Utani wa Rais Samia, matokeo kati ya Simba na Yanga

Utani wa Rais Samia, matokeo kati ya Simba na Yanga

Nukta TV

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Nukta TV