Uviko-19 kusababisha uhaba wa mabomba ya sindano?

November 22, 2021 7:37 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link

Dar es Salaam. Shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni (WHO) limesema juhudi za kuongeza uzalishaji wa chanjo dhidi ya ugonjwa wa Corona ziende sambamba na uzalishaji wa mabomba ya sindano yanayotumika kutoa chanjo hizo la sivyo kunaweza kuweko na uhaba mkubwa wa mabomba ya sindano yanayohitajika kwa ajili ya kampeni za chanjo za kawaida.

Mshauri mwandamizi wa WHO kuhusu upataji wa dawa na vifaa vya matibabu Lisa Hedman amesema kwa kuzingatia kuwa takribani watu bilioni 7 duniani kote wanahitaji dozi mbili za chanjo za Uviko-19 kati ya sasa na mwaka 2023 na kwamba kunaweza kuwapo na uhaba wa mabomba bilioni moja ya sindano.

Headman amesema kizazi kizima cha watoto kinaweza kukosa chanjo za kawaida iwapo wazalishajiwa mabomba ya sindano hatawakuwa na mpango mahsusi wa kutengeneza mabomba ya sindano ya kutumia mara moja na kutupa. 

“Unapofikiria kuhusu kiwango kikubwa cha sindano zinazotumika kwenye chanjo dhidi ya janga la Corona, hili ni jambo ambalo hupaswi kulitekeleza kwa mkato au kuweka upungufu wowote kwa ajili ya usalama wa wagonjwa na wahudumu wa afya,” amesema Headman.

Follow Us on TikTok

FOLLOW NOW

Subscribe to Our YouTube Channel

SUBSCRIBE NOW