Fahamu: Corona haidhibitiwi kwa chanjo ya nimonia

November 19, 2020 2:01 pm · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Virusi vya magonjwa hayo hushambulia mfumo wa mpumuaji.
  • WHO yasema virusi vya COVID-19 ni vipya na vinahitaji chanjo yake. 
  • Watu watakiwa kuendelea kutumia chanjo zinazopendekezwa kwa ugonjwa husika.

Dar es Salaam. Wapo baadhi ya watu wanaoamini kuwa ikiwa mtu atapata chanjo ya ugonjwa nimonia basi anajiweka katika nafasi nzuri ya kutoambukizwa ugonjwa wa Corona. Dhana hiyo siyo sahihi.

Nimonia (Pneumonia) ni ugonjwa wa mfumo wa upumuaji unaoambatana na kupungua ufanisi wa mbadilishano wa hewa kati ya binadamu na mazingira yake ya nje.

Ugonjwa huo wa homa ya mapafu huenezwa kwa njia ya hewa ama kugusana  na mgonjwa ambapo huwapata zaidi watoto na wazee kutokana na kutokuwa na mfumo imara wa kinga ya mwili. 

Licha ya kuwa virusi aina ya COVID-19 hushambulia mfumo wa upumuaji kama ilivyo kwa virusi vya nimonia, haviwezi kudhibitiwa na chanjo ya ugonjwa huo. 

Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema virusi vya COVID-19 ni vipya na vinahitaji chanjo yake isiyohusishwa na chanjo za magonjwa mengine ili kuhakikisha ufanisi wake. 

“Watafiti wanaendelea kutengeneza chanjo dhidi ya COVID-19 na WHO inazitambua na kufanikisha juhudi hizo,” imesema WHO.


Zinazohusiana:


Shirika hilo ambalo ni mwangalizi mkuu wa masuala ya afya duniani, limesema licha ya kuwa chanjo ya nimonia siyo sahihi dhidi ya COVID-19, bado linapendekeza watu kupata chanjo ya magonjwa mengine ya mfumo wa upumuaji zinazopendekezwa na wataalam wa afya ili kulinda afya zao.

Njia sahihi ya kujikinga na Corona ni pamoja na kunawa mikono mara kwa mara, kuvaa barakoa, kutumia tishu wakati kukohoa au kupiga chafya na kuepuka mikusanyiko ya watu isiyo ya lazima.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
27 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
27 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
27 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Nukta TV

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Nukta TV

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Nukta TV