Usidanganyike: Bidhaa za usafi hazitibu Corona

July 30, 2020 4:27 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Bidhaa hizo ni zile zinazotumika kuondoa uchafu kwenye vifaa, vitu na maeneo ya nyumba.
  • Bidhaa hizo hazifai kwa matumizi ya mwili na hazitibu Corona. 
  • Shirika la Afya Duniani (WHO) limeshauri bidhaa hizo kuwekwa mbali na watoto.

Dar es Salaam. Ugonjwa wa Corona umezua mengi ukiwemo uzushi kuhusu matumizi ya bidhaa mbalimbali ambazo zinadhaniwa kutibu ugonjwa wa virusi vya Corona.

Baadhi ya watu wameibuka na kudai kuwa bidhaa zinazotumika kuondoa uchafu kwenye vifaa mbalimbali (bleach na disinfectants) zinaweza kumsaidia mtu kuishinda corona pale anapokunywa au kupulizia mwili.

Shirika la Afya Duniani (WHO) limeweka wazi kuwa bidhaa hizo ni kwa ajili ya kusafisha vifaa, ngua na maeneo mbalimbali ya nyumba na siyo kwa matumizi ya mwili wa binadamu kwa kunywa au kujipulizia.


Zinazohusiana:


WHO imesema kama zitatumika kinyume na matumizi zinaweza kuleta madhara makubwa kwa binadamu na kuongeza kuwa hazitibu ugonjwa Corona.

“Kwa namna yeyote ile, usipulizie au kutumia “bleach” au “disinfectants” chochote kwenye mwili wako. Vitu hivi vinaweza kuwa sumu pale vitakapotumika kama kinywaji na kusababisha muwasho kwenye ngozi na macho,” imesema WHO. 

Pia dawa hizo zinatakiwa kuwekwa mbali na watoto ili kuepusha kunywa, jambo litakalowaweka katika hatari ya kupata matatizo ya kiafya. 

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.