Usidanganyike: Bidhaa za usafi hazitibu Corona
- Bidhaa hizo ni zile zinazotumika kuondoa uchafu kwenye vifaa, vitu na maeneo ya nyumba.
- Bidhaa hizo hazifai kwa matumizi ya mwili na hazitibu Corona.
- Shirika la Afya Duniani (WHO) limeshauri bidhaa hizo kuwekwa mbali na watoto.
Dar es Salaam. Ugonjwa wa Corona umezua mengi ukiwemo uzushi kuhusu matumizi ya bidhaa mbalimbali ambazo zinadhaniwa kutibu ugonjwa wa virusi vya Corona.
Baadhi ya watu wameibuka na kudai kuwa bidhaa zinazotumika kuondoa uchafu kwenye vifaa mbalimbali (bleach na disinfectants) zinaweza kumsaidia mtu kuishinda corona pale anapokunywa au kupulizia mwili.
Shirika la Afya Duniani (WHO) limeweka wazi kuwa bidhaa hizo ni kwa ajili ya kusafisha vifaa, ngua na maeneo mbalimbali ya nyumba na siyo kwa matumizi ya mwili wa binadamu kwa kunywa au kujipulizia.
Zinazohusiana:
- Jinsi ya kuthibitisha habari za Corona unapotumia Twitter
- Unaandaa sherehe ya harusi wakati wa corona? Zingatia haya
- Google inavyowezesha uthibitishaji wa taarifa za Corona mtandaoni
WHO imesema kama zitatumika kinyume na matumizi zinaweza kuleta madhara makubwa kwa binadamu na kuongeza kuwa hazitibu ugonjwa Corona.
“Kwa namna yeyote ile, usipulizie au kutumia “bleach” au “disinfectants” chochote kwenye mwili wako. Vitu hivi vinaweza kuwa sumu pale vitakapotumika kama kinywaji na kusababisha muwasho kwenye ngozi na macho,” imesema WHO.
Pia dawa hizo zinatakiwa kuwekwa mbali na watoto ili kuepusha kunywa, jambo litakalowaweka katika hatari ya kupata matatizo ya kiafya.
Latest
