Unaishi Rukwa? Chanjo ya Uviko-19 inatolewa katika vituo hivi
Dar es Salaam. Kama uko katika Mkoa wa Rukwa iwe mjini au vijijini na una sifa za kupata chanjo ya Corona, Serikali imeweka vituo 11 katika Halmashauri nne za mkoa huo ili kutoa fursa kwa watu kuchanjwa.
Nenda kachanje ili uwe salama. Kumbuka chanjo husaidia kumkinga mtu na maambukizi ya ugonjwa wa Uviko-19. Kwa sasa, Tanzania inatumia chanjo aina ya Johnson & Johnson ambayo mtu anayechanjwa anapatiwa dozi moja tu.
