Umaskini unavyowatesa watoto duniani

March 15, 2022 8:30 am · Herimina
Share
Tweet
Copy Link

                   


  • Takriban watoto bilioni 1 duniani wanaishi katika umaskini wa kukosa mahitaji yao muhimu.
  • Watoto  milioni 150 waongezeka katika kundi hilo kutokana na Uviko-19.
  • Watoto hao wapo hatarini kupoteza maisha na kuwa na maisha duni ukubwani.

Dar es salaam. Umaskini wa mtoto  bado ni changamoto kubwa duniani licha ya uwepo wa harakati za kutokomeza umaskini katika mataifa mbalimbali.

Hali hiyo inayomfanya mtoto kuishi katika mazingira duni, husababisha mtoto kukosa mahitaji ya msingi ikiwemo chakula, malazi, huduma za afya na elimu.

Shirika la kuhudumia watoto duniani (UNICEF) limesema kuwa takriban watoto bilioni 1 duniani wanaishi katika umaskini wa kukosa mahitaji yao muhimu, huku watoto milioni 150 wakiongezeka katika kundi hilo kutokana na Uviko-19.

Japo kuna watoto ambao wanapata mahitaji hayo, bado wanawekwa katika kundi hili kutokana na kiwango cha mahitaji wanayopata kuwa duni, ikiwemo kula chakula kisicho na lishe bora, na kutumia maji yasiyo safi na salama.

Takriban  asilimia 88 ya watoto wanakosa zaidi ya mahitaji matatu muhimu, huku zaidi ya nusu  wakikosa mahitaji hayo zaidi ya matano. Picha| Nukta Habari.

Watoto wengine wanaishi katika umaskini uliokithiri katika nyanja zote kwa kukosa mahitaji matatu au zaidi ya lishe, ulinzi, elimu, kupata na kutoa taarifa, maji, makazi, afya, na mazingira safi.

Kwa Tanzania, takriban  asilimia 88 ya watoto wanakosa zaidi ya mahitaji matatu muhimu, huku zaidi ya nusu  wakikosa mahitaji hayo zaidi ya matano, kwa mujibu wa Ripoti ya umaskini wa mtoto Tanzania  ya mwaka 2019 iliyotolewa na UNICEF pamoja na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS). 

Hali hiyo inaweweka watoto hawa hatarini mara mbili zaidi kupoteza maisha wakiwa watoto ikilinganishwa na watoto ambao si maskini.


Zinazohusiana:


UNICEF inaeleza kuwa licha ya watoto kuwa theluthi moja ya idadi yote ya watu duniani, kundi hilo linachukua nusu ya watu wanaotumia chini ya dola 1.9 kwa siku  sawa na shilingi za Kitanzania 4,300, huku  watoto milioni 365 wakiishi katika umaskini uliopindukia.

Shirika hilo linaongeza kuwa watoto wanaokuwa katika umaskini huteseka ukubwani  kwa kuwa na maisha duni, ujuzi kidogo wa kazi, na kufanya kazi za mishahara ya chini.

Jambo linalohuzunisha zaidi ni kuwa, licha ya hali hiyo, ni mataifa machache ndiyo yameweka mkazo kutokomeza umaskini kwa watoto kama kipaumbele cha Taifa.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
25 Aug, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
25 Aug, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Elimu ya kodi mwarobaini wa wafanyabiashara kuikwepa TRA, ianzie shuleni

Elimu ya kodi mwarobaini wa wafanyabiashara kuikwepa TRA, ianzie shuleni

Nukta TV

Rais Samia: Serikali chini ya Magufuli haikutaka kuyumbishwa kukamili kwa JNHPP

Rais Samia: Serikali chini ya Magufuli haikutaka kuyumbishwa kukamili kwa JNHPP

Nukta TV

Rais Samia: Umeme wa SGR hautoingiliwa, Dodoma umeme uhakika 24/7

Rais Samia: Umeme wa SGR hautoingiliwa, Dodoma umeme uhakika 24/7

Nukta TV