Ujumbe wa Rais Samia kwa Watanzania mwaka 2023
Dar es Salaam. Mbali na Rais Samia Suluhu Hassan kuwataka Watanzania kusherehekea sikukuu za mwisho wa mwaka kwa amani na utulivu pia amewataka kuendelea kufanya kazi kwa juhudi na weledi watakapoingia mwaka 2023 ili nchi iendelee kupiga hatua mbele.
Rais Samia ametoa ujumbe huo wa heri kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Twitter wakati wakristo nchini wanaungana na wengine duniani kuadhimisha sikukuu ya Krismas ya kuzaliwa kwa Yesu.
“Nawatakia Watanzania wote kheri ya Krismasi na Mwaka Mpya. Tumpe Mwenyezi Mungu shukrani kwa kutufikisha salama wakati huu wa mwaka,” amesema Rais.
Nawatakia Watanzania wote kheri ya Krismasi na Mwaka Mpya. Tumpe Mwenyezi Mungu shukrani kwa kutufikisha salama wakati huu wa mwaka. Tusherehekee kwa amani, upendo na kiasi. Mwaka 2023 tukaendelee kufanya kazi kwa juhudi na weledi, ili nchi yetu iendelee kupiga hatua mbele zaidi.
— Samia Suluhu (@SuluhuSamia) December 25, 2022
Latest