Mwelekeo wa Serikali ya Rais Samia mwaka 2022

January 1, 2022 7:40 am · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni kukabiliana na changamoto za wananchi.
  • Kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja.
  • Kuendeleza mapambano dhidi ya janga la Uviko-19.

Dar es Salaam. Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ameanika mipango ya Serikali yake kuelekea mwaka 2022 ambayo imejikita katika kuimarisha ustawi wa Watanzania kiafya na kiuchumi.

Rais Samia amesema hayo wakati akihutubia Watanzania kwa njia ya televisheni leo Desemba 31, 2022.

Amesema 2022 ni mwaka wa kukabiliana na changamoto zinazopunguza uwezo wa wananchi katika kukabiliana na maisha ya kila siku ili kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja na wa Taifa kwa ujumla.

Amesema dunia inakabiliwa na ugonjwa wa Corona (Uviko-19) na itaendeleza mapambano ya ugonjwa huku akiwataka wananchi kuchukua tahadhari kwa sababu wimbi la nne la ugonjwa huo na kirusi cha Omicron tayari kimeshaingia Tanzania.

“Nitumie fursa hii kuwahimiza wananchi kupata chanjo dhidi ya Uviko 19, natambua kuwa chanjo haizuii mtu kupata maambukizi ila inapunguza makali ya ugonjwa huu. Hivyo niwakumbushe wananchi kwenda, chanjo zipo na zinapatikana bila malipo,” amesema Rais.


Soma zaidi:


Eneo lingine litakalopewa kipaumbele na Serikali ya Tanzania ni kuhakikisha zoezi la Sensa ya Watu na Makazi linafanikiwa kwa kuhakikisha watu wote wanahesabiwa ili kupata takwimu zitakazosaidia kufanya maamuzi sahihi ya maendeleo.

Amesema sensa itasaidia upatikanaji wa takwimu zitakazosaidia serikali kupanga kwa usahihi mipango ya maendeleo.

“Ni vyema tukauanza mwaka mpya2022 na lengo la kuongeza ufanisi katika uzalishaji na ubora katika kutoa huduma,” amesema Rais Samia akiwasihi wafanyakazi wa sekta ya umma na binafsi.


Wito kwa wazazi

Amewataka wazazi kutokubweteka na msimu wa sikukuu na sherehe zake na badala yake kuwaandaa watoto wao kukabiliana na changamoto za masomo katika mwaka u ujao ili waweze kunufaika na elimu inayotolewa.

Amewataka wanaosafiri msimu huu wa mwisho wa mwaka kuzingatia sheria za usalama barabarani ili kupunguza ajali na kuokoa nguvukazi ya Taifa inayotegemewa katika uzalishaji.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Nukta TV

Rais Samia: Kalamu yangu ina hatari, sijawahi kusaini mtu kunyongwa

Rais Samia: Kalamu yangu ina hatari, sijawahi kusaini mtu kunyongwa

Nukta TV

Rais Samia: Matumizi jina Samia, likiwa kila mahali inachosha, tafuteni wengine

Rais Samia: Matumizi jina Samia, likiwa kila mahali inachosha, tafuteni wengine

Nukta TV