Uamuzi mgumu UN: Nani apatiwe msaada wa chakula Afrika Mashariki?

April 14, 2022 5:13 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Mamilioni ya wakimbizi wa Mashariki mwa Afrika wako hatarini kutumbukia kwenye njaa kali.
  • Ni baada ya mgao wa chakula kupungua.
  • UNHCR, WFP zahaha kugawa chakula kilichopo kwa wakimbizi zaidi ya milioni 5. 

Dar es Salaam. Mamilioni ya familia za wakimbizi katika eneo la Mashariki mwa Afrika ikiwemo Tanzania ziko hatarini kutumbukia kwenye njaa kali wakati huu ambapo mgao wa chakula unapungua kutokana na rasilimali za misaada ya kibinadamu kuzidiwa uwezo. 

Hali hiyo imesababishwa na  madhara ya tabianchi, janga la Uviko-19 na ongezeko la bei ya chakula na mafuta, yamesema mashirika mawili ya Umoja wa Mataifa, lile la kuhudumia wakimbizi (UNHCR) na mpango wa chakula duniani (WFP). 

Mashirika hayo katika taarifa ya pamoja iliyotolewa April 13 Geneva, Uswisi yamesema, licha ya juhudi za kuhakikisha chakula kilichopo kinapatiwa familia kwa misingi ya kipaumbele cha uhitaji, idadi ya wakimbizi wenye uhitaji inaongezeka, sambamba na pengo la rasilimali zilizopo. 

Wakimbizi hao wako katika nchi za Burundi, Djibouti, Ethiopia, Kenya, Rwanda, Sudan Kusini, Sudan, Tanzania na Uganda. 

Katika kipindi cha muongo mmoja uliopita, idadi ya wakimbizi Mashariki mwa Afrika imeongezeka mara tatu kutoka milioni 1.82 mwaka 2012 hadi takribani milioni 5 Aprili mwaka huu, ikiwemo wakimbizi wapya 300,000 wa mwaka jana pekee. 

WFP imesema ongezeko la idadi ya wakimbizi isiyoendana na chakula kinachopatikana kinaliacha shirika hilo na uamuzi mgumu wa nani apatiwe msaada wa chakula na nani anyimwe.

 “Leo hii asilimia 70 ya wakimbizi wenye uhitaji hawapokei mgao kamili wa chakula kutokana na ukata,” amesema Clementine Nkweta-Salami, Mkurugenzi wa UNHCR kwa kanda ya Mashariki, Pembe ya Afrika na Maziwa Makuu. 


Soma zaidi:


Amesema watoto wengi zaidi wenye umri wa chini ya miaka 5 wanakumbwa na viwango vya juu vya udumavu na ukuaji usiondana na umri wao kwa kuwa hawana lishe bora na virutubisho vinavyotakiwa wakati wanakua. 

“Familia hazijui mlo ufuatao unatokana wapi na wanakumbwa na deni kubwa, wanauza mali zao na hata kuwaondoa watoto wao shulen ili washiriki katika kazi. Hii inaongeza hatari ya ukatili wa majumbani. Kuwaondoa watu kwenye hatari hii inapaswa mahitaji yao ya chakula yaweze kukidhiwa.

“Ukweli wa kusikitisha ni kwamba eneo la Mashariki mwa Afrika linakumbwa na mahitaji ya aina yake ya kibinadamu, yakichochea na mabadiliko ya tabianchi, mizozo, ukosefu wa utulivu na ongezeko la bei za vyakula na nishati ya mafuta,” amesema Michael Dunform, Mkurugenzi wa WFP kanda ya Mashariki mwa Afrika. 

Amesema ongezeko la mahitaji kwenye ukanda huo linaakisi kile kinachoonekana pia duniani kote, “hivyo tunaomba dunia isiipe kisogo eneo hili na hususan jamii zilizo hatarini zaidi za wakimbizi ambazo zina fursa finyu ya mbinu za kujipatia kipato na tegemeo lao kuu ni WFP ili ziweze kuishi.” 

WFP kwa kuanzia kipindi cha mwezi Aprili hadi Septemba mwaka huu wa 2022, inahitaji dola milioni 226.5 (Sh525.8 bilioni kukidhi mgao kamilifu wa chakula kwa wakimbizi katika nchi zilizoko Mashariki mwa Afrika. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV