Zaidi ya watu milioni 50 kukumbwa na balaa la njaa Afrika Mashariki

July 23, 2022 11:45 am · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Zaidi ya watu milioni 50 kukumbwa na balaa la njaa Afrika Mashariki
  • Ni kutokana na kupungua kwa uzalishaji wa mazao.
  • Mabadiliko ya tabianchi nayo yachangia.

Dar es Salaam. Zaidi ya watu 50 milioni waishio nchi za Afrika Mashariki kukabiliwa na janga la njaa kwa mwaka 2022, huku sababu kubwa ikiwa ni mabadiliko ya tabia ya nchi, migogoro na changamoto za kiuchumi.

Taarifa ya pamoja ya Shirika la Chakula na Kilimo  Duniani (FAO),  Mpango wa Chakula wa Dunia (WPF) na Mamlaka ya Maendeleo ya Kiserikali (IGAD) iliyotolewa  Julai 22, mjini Addis Ababa, Ethiopia,  inasema Ethiopia, Kenya, Somalia, Sudan Kusini, na Sudan ndiyo nchi zilizoathirika zaidi na balaa hili.

“Takwimu tunazotoa  ni za kuhuzunisha, na nina wasiwasi kwamba zinaweza kuongezeka zaidi kwani matarajio ya msimu wa mvua wa Oktoba hadi Desemba ni mbaya.” amesema Workneh Gebeyehu, Katibu Mtendaji IGAD.

Taarifa hiyo inafafanua zaidi kuwa janga  la njaa kwa mwaka 2022 limeongezeka kwa asilimia 19, ukilinganisha  idadi ya watu  milioni 42 iliyokubwa na janga la njaa kwa  mwaka 2021.

Sambamba na hilo takriban watu 300,000 wanatarajiwa kukabiliwa na janga la njaa la juu ngazi ya tano  hususani kwenye nchi za Somalia na Sudan Kusini.

Sababu kubwa ni kushindwa kwa uzalishaji wa mazao na mifugo, kuongezeka kwa gharama za chakula na kukosekana kwa misaada ya kibinadamu.

Janga hilo pia limewakumba watoto  milioni 10 walio chini ya umri wa miaka 5, huku wakikabiliwa na utapiamlo mkali.


Soma zaidi:


Tanzania hali ikoje

Wakati baadhi ya Watanzania wakila na kusaza kiasi cha kutupa chakula, ripoti mpya ya usalama wa chakula na lishe Tanzania inakadiria kuwa kuanzia Mei 2022 watu 592,000 watakabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula kutokana na kushuka kwa uzalishaji wa mazao ya chakula katika baadhi ya maeneo nchini. 

Kufahamu zaidi, sikiliza sauti hii kuhusu hali ya chakula nchini Tanzania:

           

Follow Us on TikTok

FOLLOW NOW

Subscribe to Our YouTube Channel

SUBSCRIBE NOW