Thamani ya hisa za Kenya Airways zashuka soko la hisa Dar

October 16, 2019 3:22 am · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Hadi soko linafungwa leo jioni, thamani hisa moja ya KA ilikuwa Sh55 kutoka Sh60 iliyorekodiwa jana sawa. 
  •  Wawekezaji wa kampuni hiyo wamepoteza Sh5 kwa kila hisa moja leo sokoni.
  • Thamani ya hisa za kampuni za NMG na EABL zapanda kwa viwango tofauti. 

Dar es Salaam. Thamani ya hisa za kampuni ndege la Kenya Airways (KA) katika soko la hisa la Dar es Salaam (DSE) imeshuka kwa asilimia 8.33 na kuwafanya wawekezaji waliowekeza katika kampuni hiyo kupoteza Sh5 kwa kila hisa.

Ripoti ya siku iliyotolewa leo (Oktoba 15, 2019) na DSE inaeleza kuwa hadi soko linafungwa leo jioni, thamani hisa moja ya KA ilikuwa Sh55 kutoka Sh60 iliyorekodiwa jana. 

Hiyo ina maana kuwa wawekezaji wa kampuni hiyo watalala na maumivu kwa sababu wamepoteza Sh5 kwa kila hisa moja leo sokoni.

Wakati thamani ya hisa za KA ikishuka, kampuni ya habari ya NMG na kampuni ya bia ya Afrika Mashariki (EABL) zina kila sababu ya kutabasamu kwa sababu thamani ya hisa zao zimepanda kwa viwango tofauti. 

Thamani ya hisa za NMG zimepanda kwa asilimia 2.20 ambapo mpaka soko linafungwa thamani ya hisa moja ilikuwa Sh930 kutoka Sh910 iliyorekodiwa jana na kuweka kibindoni Sh20 kwa kila hisa.

EABL nayo thamani ya hisa zake zimepanda kwa asilimia 0.47 hadi kufikia Sh4,260 leo jioni ukulinganisha na jana ambapo thamani yake ilikuwa Sh4,240. 


Zinazohusiana: 


Wakati thamani ya hisa za NMG na EABL zikipanda na zile za KA zikishuka, kampuni zilizobaki viwango vyake vibaki kama vilivyokuwepo jana zikiwemo Vodacom, na benki ya CRDB, DCB na Acacia. 

Hata hivyo, benki ya CRDB ndiyo iliyofanya vizuri zaidi leo baada ya kuongoza kwa kuuza kiwango kikubwa cha hisa. 

Vodacom imeuza hisa 66,905 sawa na asilimia 92.3 ya hisa zote zilizouzwa sokoni leo huku ikifuatiwa kwa mbali na kampuni ya uwekezaji ya  NICO ambayo imeuza hisa 5,000 na kampuni ya bia ya TBL (500).

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV