Rais Samia atoa pole ajali ya kuporomoka jengo Kariakoo

November 16, 2024 1:45 pm · Esau Ng'umbi
Share
Tweet
Copy Link
  • Aaagiza viongozi, vyombo vya ulinzi na usalama  pamoja na Jeshi la Uokozi kufanikisha zoezi la uokozi na tiba.
  • Awataka Watanzania kuwaombea majeruhi na kuwatia moyo wafanyabiashara walioathirika na ajali hiyo

Dar es Salaam. Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ametoa pole kwa Watanzania na wafanyabiashara kufuatia ajali ya kuanguka kwa ghorofa iliyotokea leo Novemba 16, 2024 katika Mtaa wa Kongo, Manyema na Mchikichi Dar es Salaam.

Jengo hilo linaelezwa kuporomoka majira ya saa tatu asubuhi ambapo kwa mujibu wa mashuhuda waliozungumza na Shirika la Utangazaji Tanzania ( TBC) ndani ya jengo hilo la kibiashara, kulikuwa na watu kadhaa waliokuwa wakifanya ununuzi katika maduka ya jengo hilo.

Rais Samia aliyesafarini kuelekea nchini Brazil kuhudhuria mkutano wa G20 ametoa salamu za pole kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii ambapo amesema amesikitika kupokea taarifa ya ajali hiyo na kuwa ameshaagiza viongozi, vyombo vya ulinzi na usalama  pamoja na Jeshi la Uokozi kufanikisha zoezi la uokozi na tiba.

“Nimeuagiza Uongozi wa Mkoa wa Dar es Salaam, Jeshi la Polisi, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Uongozi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, na Idara ya Menejimenti ya Maafa kufanya kila linalowezekana kufanikisha zoezi la uokoaji na tiba kwa majeruhi,” ameeleza Rais Samia.

Aidha Rais Samia amewataka Watanzania kuwaombea majeruhi kupata nafuu haraka hpamoja na kuwaombea subra ndugu jamaa, marafiki wanaotafuta riziki zao katika soko hilo la kimataifa.

kwa mujibu wa mashuhuda wa ajali hiyo aliyekuwa akizungumza na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), ghorofa hilo limeanguka ghafla majira ya saa 3:05 asubuhi wakati mafundi wa ujenzi walipokuwa kazini wakitoboa kwa ajili ya kuongeza sehemu ya maduka chini ya jengo hilo.

“Tulianza kusikia kelele za mtingishiko, kisha kwa ghafla jengo zima likaanguka, wananchi wameshindwa kujiokoa na kazi ya ujenzi ilianza tangu jana, hivyo angetaka urahisi angebomoa tu jengo lote,” amesema mmoja wa mashuhuda, Harrison Shayo.

Shughuli ya uokoaji inaendelea kwa wananchi wakishirikiana na vyombo vya dola ikiwemo Jeshi la Zimamoto na Uokoaji ambapo hadi saa 5 asubuhi bado hakuna taarifa ya moja kwa moja juu ya athari zilizosababishwa na kuporomoka kwa jengo hilo.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila aliyekuwa akizungumza na wananchi na wanahabari katika eneo hilo amesema majeruhi waliookolewa wamefikishwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Hata hivyo, amesema hadi sasa idadi ya majeruhi haijafahamika wala waliopoteza maisha, akisisitiza takwimu rasmi zitatolewa baadaye.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
13 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
14 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
14 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

Nukta TV

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Nukta TV

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Nukta TV