Thamani miamala ya kifedha kwa njia ya simu yapungua, watumiaji wakiongezeka

October 27, 2022 1:36 pm · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Yapungua kwa Sh19.09 bilioni ndani ya mwezi mmoja.
  • Watumiaji na idadi ya miamala waliyofanya yaongezeka. 

Dar es Salaam. Ripoti mpya ya Takwimu za Mawasiliano ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) inaonyesha kuwa miamala inayofanywa kupitia huduma za kifedha za simu za mkononi imepungua kwa Sh19.09 bilioni ndani ya mwezi mmoja.

Ripoti hiyo ya robo ya tatu ya mwaka 2022, inabainisha kuwa mwezi Septemba pekee thamani ya miamala ya fedha iliyofanywa katika simu za mkononi ilikuwa Sh12.72 trilioni kutoka Sh12.74 trilioni iliyorekodiwa Agosti mwaka huu.

Huduma za kifedha za kwenye simu zinasaidia kuongeza mzunguko wa fedha nchini na kutatua changamoto mbalimbali za kibenki ikiwemo kuweka fedha, kukopa na kulipia huduma na bidhaa mbalimbali.

Licha ya thamani ya miamala hiyo kupungua, miamala kwa njia ya simu iliyofanywa Septemba imeongezeka hadi milioni 366.17 kutoka miamala milioni 356.79 ya mwezi uliotangulia. 

Kwa wastani Septemba mtu mmoja alikuwa anafanya miamala ya kifedha tisa kwenye simu yake yenye thamani ya 321,341. 

TCRA katika ripoti hiyo, imeeleza kuwa idadi ya watumiaji wa huduma za kifedha kwa njia ya simu imeongezeka hadi watu milioni 39.5 Septemba mwaka huu kutoka watumiaji milioni 38.5 wa mwezi Agosti.

Kampuni ya Vodacom inayomiliki M-Pesa ndiyo inamiliki sehemu kubwa ya soko la huduma za kifedha kwa njia ya simu kwa asilimia 39 ikifuatiwa na Tigo (asilimia 25) na Airtel kwa asilimia 23. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV