Taarifa muhimu kuhusu virusi vya Corona

March 16, 2020 10:00 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Mpaka sasa virusi hivyo vimethibitishwa katika nchi 22 za Afrika.
  • Rwanda na Kenya zimekuwa nchi za kwanza Afrika Mashariki kupata wagonjwa wa virusi hivyo. 

Wakati hakuna mgonjwa yeyote aliyebainika kuwa ugonjwa wa virusi vya Corona  Tanzania,  nchi kadhaa ya Afrika zimeifunga mipaka na kuweka vizuizi katika safari za ndege kwa lengo la kuzuia kuenea kwa virusi vya corona ambavyo vimekwishathibitishwa katika nchi 26 za bara hilo.

Kati ya nchi hizo zipo mbili za Afrika Mashariki za Rwanda na Kenya.  

Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa ametangaza hali ya dharura kitaifa, na kuonya kuwa janga la virusi hivyo linaweza kuwa na athari za kudumu kwa uchumi wa nchi yake. 

Naye Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta pia amepiga marufuku safari za ndege kutoka nchi zote ambako maambukizi ya virusi vya Corona (COVID-19) yamekwisharipotiwa.

Shule na vyuo vikuu vimefungwa katika mataifa mengi ya Afrika sambamba na mikusanyiko yote ya hadhara, ikiwemo ya kidini. 

Inaelezwa nchini Ghana, Rais Nana-Akufo Addo ameamuru shughuli za mazishi zisihudhuriwe na watu zaidi ya 25.

Licha ya kuwa ugonjwa huo kuendelea kueneo katika maeneo mbalimbali duniani, Watanzania wametakiwa kuchukua tahadhari ya kujikinga na maambukizi ikiwemo kuosha mikono mara kwa mara hasa baada ya kushika vitu katika maeneo yenye watu wengi. 

Pia Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) linawataka watu kutokugusa mdomo, macho au pua na kutakiwa kutumia tishu wakati wa kukohoa ua kupiga chafya. Baada ya matumizi tishu inatakiwa kutupwa sehemu salama. 

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.