Simu za mkononi: Mbadala wa masanduku ya posta

May 5, 2022 1:00 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Zitatumika kuboresha masanduku hayo ya posta.
  • Vifurushi kuwafikia wateja popote walipo kwa kutumia simu za mkononi.

Mwanza. Huenda huduma za kupokea na kutuma barua na vifurushi zikamfikia kila mtumiaji wa simu Tanzania, baada ya huduma za posta kuunganishwa na mtandao wa simu nchini.

Shirika Posta Tanzania (TPC)  limesema kukamilika kwa usajili wa makazi kunaenda sambamba na uboreshaji wa anuani za masunduku ya posta ambapo namba za simu zitatumika kama mbadala wa anuani hizo.

Meneja wa TPC Mkoa wa Mwanza na Geita,  Dongwe James  akizungumza leo Mei 5, 2022 jijini Mwanza, amesema maboresho hayo yatarahisisha  shughuli za maendeleo  na kuimarisha ulinzi na usalama wa Taifa.

“Zamani watumiaji wa posta walikuwa wanaandika anuani ya posta pekee, hivi sasa tumeboresha kuendana na mabadiliko ya teknolojia,  mteja anapotuma bahasha yake posta ataandika anuani yake,  namba ya nyumba anayoishi na simu yake ya mkononi na mzigo wake atafikishiwa mpaka mlangoni,” amesema Dongwe.


Soma zaidi: 


Amesema anuani za makazi na ukuaji wa teknolojia ni muhimu kwa usalama wa Taifa na watumiaji wa huduma za posta kote duniani.

Meneja huyo amewataka wananchi kutoa ushirikiano kwa watendaji wanaotekeleza suala hilo ili kwenda sambamba na maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha zoezi la anuani na makazi.

Wakizungumza na Nukta habari baadhi ya wakazi jijini Mwanza wamepongeza jitihada zinazofanywa na shirika hilo na kwamba zitasaidia katika kurahisisha utoaji wa huduma.

Abel  Nkurumba, mkazi wa jijini hapa amesema zaman walipopeleka mzigo au barua walilazimika kusubiri miezi au wiki ndipo mzigo ufike lakini hivi sasa ndani ya masaa 24 au 48 unapata mzigo wako.

“Huduma zimerahisishwa ni tofauti na zamani na hii ya anuani za makazi itaongeza urahisi wa mzigo au kifurushi kufika bila kupotea,” amesema Nkurumba.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.