Wanaoumwa kipindupindu Mwanza wafikia 80

January 16, 2024 2:06 pm · Mariam John
Share
Tweet
Copy Link
  • Waongezeka kutoka 34 walioripotiwa wiki moja iliyopita.
  • Jamii yaonywa kuzingatia kanuni za afya, kuacha dhana potofu.

Mwanza. Licha ya juhudi za kukabiliana na ugonjwa wa kipindupindu zinazoendelea mkoani Mwanza, idadi ya watu wanaougua ugonjwa huo imeongezeka na kufikia 80, tangu ugundulike kuwepo jiji hilo la Kanda ya Ziwa Januari 4, 2024.

Hii ni mara ya tatu kwa visa vya ugonjwa huo kuongezeka kwa kuwa Januari 10, 2024, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dk. Thomas Rutachunzibwa alitangaza idadi ya wagonjwa kufikia 34 ambaao waliongezeka kutoka saba walioripotiwa awali.

Kwa mujibu wa Waziri wa Afya Ummy Mwalimu mpaka Januari 12, 2023 mikoa 6 ya Mwanza, Shinyanga, Ruvuma, Tabora, Simiyu na Kagera tayari ilikuwa inakabiliwa na ugonjwa huo.


Soma zaidi : Unavyoweza kuepuka ugonjwa wa ‘red eyes’


Pamoja na hatua za kiafya zilizochukuliwa ikiwa ni pamoja na kuzuia matanga ya muda mrefu,  Dk. Rutachunzibwa ametoa wito kwa vyombo vya habari kuendelea kutoa elimu kwa umma kuhusiana na namna ya kujikinga na ugonjwa huo ili kuepukana na maambukizi zaidi.

“Kwa sasa tunatazama zaidi mikusanyiko ya misiba kwa kuwa ndipo kwenye chanzo cha maambukizi hayo na tunashauri unapotokea msiba ni vyema jamii ikashiriki kwenye mazishi pekee na kusambaa,” amesema Dk. Rutachunzibwa.

Mikakati mingine inayotekelezwa ni pamoja na kuhamasisha jamii kula chakula cha moto, pamoja na kunywa safi maji yaliyochemshwa au kutibiwa kwa kidonge kinachosambazwa cha Aquatabs.

“Kidonge hiki kimoja kinatumika kutibu ndoo ya lita 10 na viwili kwa ndoo ya lita 20, na kidonge hichi kinatakiwa kuhifadhiwa sehemu isiyokuwa na mwanga mkali kwa kuwa kikiachwa hapo kinaweza kusababisha madhara mengine ya kiafya,” amesema Dk. Rutachunzibwa.

Maji yaliyogandishwa hayaui vimelea

Renald Mlyakado ambaye ni Mratibu wa Elimu ya Afya kwa Umma, aliyekuwa akitoa elimu kwa waandishi wa habari, ameitaka jamii kuondoa dhana potofu kuwa, kuweka maji kwenye jokofu  au kuyaacha kwenye ndoo kwa muda mrefu yanasababisha wadudu kuganda na kufa.

Mlyakado amedai dhana hiyo sio ya kweli badala yake, wadudu husinyaa tu kwa muda na iwapo mtu atatumia maji yenye vimelea yaliyokaa muda mrefu atakuwa hatarini kupata kipindupindu.

“Kwahiyo tusidanganyike kuwa kuweka maji kwenye friji kunaua wadudu hao hapana, tunachoshauri ni mtu kuchemsha maji na kuyahifadhi vizuri kabla ya kuyatumia,” amesema Mlyakado

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
21 May, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
21 May, 2026
No active movers today
Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: ULEGA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA UJENZI BUNGENI

🔴LIVE: ULEGA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA UJENZI BUNGENI

Nukta TV

NMB BANK YATANGAZA GAWIO LA SH610 KWA HISA 2025

NMB BANK YATANGAZA GAWIO LA SH610 KWA HISA 2025

Nukta TV

🔴LIVE: ULEGA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA UJENZI BUNGENI

🔴LIVE: ULEGA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA UJENZI BUNGENI

Nukta TV