Sekta binafsi kuwabeba wamachinga Tanzania

May 21, 2022 7:28 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Yatakiwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya biashara wamachinga. 

Dar es Salaam. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Innocent Bashungwa, ameitaka sekta binafsi na washirika wa maendeleo kushirikiana na Serikali kuwatengenezea mazingira wezeshi wafanyabiashara ndogo (Wamachinga) ili waweze kukuza biashara zao na kuchangia katika ukuaji wa uchumi wa Taifa.

Bashungwa aliyekuwa akizungumza Mei 20, 2022 jijini Dodoma wakati akifungua warsha ya wamachinga iliyoandaliwa na Wizara ya Fedha na Mipango kwa ushirikiano na Mfuko wa Uendelezaji wa Sekta ya Fedha nchini (FSDT) amesema kundi hilo linahitaji kupewa kipaumbele nchini.

“Wamachinga wakijenjengewa mazingira mazuri yatakayowawezesha kukuza mitaji yao, ni fursa nzuri kwa mabenki kwa kuwa yatakuwa na wateja wa kuwakopesha,” amesema Bashungwa.

Wadau waliohudhuria warsha hiyo wametakiwa kufanya uchambuzi wa maeneo yanayofanya vizuri kwa wamachinga, changamoto na fursa ili kujua wajibu wa kila mmoja katika kuhakikisha wafanyabiashara hao wanakua na kuleta tija stahiki kwa Taifa.

Kwa sasa, Serikali iko mbioni kutunga sheria itakayosimamia shughuli na maslahi ya wamachinga nchini ili kuwasaidia Watanzania waliojiajiri katika sekta hiyo isiyo rasmi kuboresha maisha yao.

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mwanaidi Ali Khamis amesema kuwa shughuli za machinga zimesaidia kutatua changamoto za ajira kwa vijana kwa kujiajiri na kuwa sehemu ya ukuaji wa uchumi wa nchi.

Kutokana na umuhimu huo, amesema  Serikali imechukua hatua mbalimbali kuhakikisha kuwa kundi la wamachinga linahudumiwa kwa upekee kwa kuratibu shughuli wanazozifanya ili ziweze kuwanufaisha na kuwaletea maendeleo.


Zinazohusiana:


Bajeti ya 2022/23 kuwajumuisha wamachinga

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Lawrence Mafuru, amesema kuwa wizara yake ipo katika hatua za kutengeneza Bajeti Kuu ya Serikali ambapo itawajumuisha wamachinga katika utekelezaji wake.

Amesema kuwa warsha ya wamachinga itasaidia kutoa fursa ya kujifunza lakini pia kuwa na sera itakayoelekeza rasilimali fedha kutoka kwa wadau mbalimbali inapatikanaje kwa ajili ya eneo hilo.

Eneo la wamachinga linahudumiwa na wizara nyingi ikiwemo Tamisemi, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum pia katika maeneo ya kiutawala kama Mikoa na Wilaya.

Mafuru ameshauri kuwa na muelekeo mmoja kama Serikali badala ya kulishugulikia suala hilo kwa uelewa wa mtu mmoja mmoja, hivyo warsha hiyo ni muhimu katika kupata maoni ya wadau.

Mwenyekiti wa Wamachinga Taifa, Ernest Masanja,amesema kuwa kundi la wamachinga lilitengwa lakini sasa linashirikiana vizuri na Serikali hivyo akaahidi wamachinga kuiunga mkono Serikali katika jitihada zake za maendeleo.

Warsha hiyo imewakutanisha makatibu wakuu wa kisekta, wakuu wa mikoa, makatibu tawala wa mikoa, wakuu wa wilaya, wakuu wa idara, viongozi wa wamachinga na wadau wengine.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.